• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DC Morogoro amtaka Chifu Kingalu kusimamia Mila za Kiluguru

Posted on: November 6th, 2018

Na. Andrew Chimesela  - Morogoro


Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Bi Regina Chonjo amemtaka Chifu wa kabila la Waluguru Mkoani Morogoro Chifu Kingalu Mwanabanzi wa 15 kusimamia na kutunza mila na desturi za kabila hilo ili kurithisha kizazi cha sasa na kijacho utamaduni wa kabila hilo.


Mkuu huyo wa Wilaya ametoa ushauri huo leo Novemba 6 mwaka huu wakati akikabidhi vifaa vya mila na desturi vya kabila la waluguru ambavyo vilipotea miaka 30 iliyopita katika mazingira ya kutatanisha ambavyo sasa vimepatikana baada ya Mkuu huyo wa Wilaya kuwaita Wazee wa Mila na Desturi Mkoa wa Morogoro kufika Ofisini kwake ili kuvitambua vifaa hivyo.


Bi. Regina Chonjo amesema ni vema vifaa hivyo vilivyokuwa vimepotea vitunzwe na kufanya kazi yake na si kuvihifadhi pekee ili kuendelea kutunza utamaduni wa kabila la Waluguru, historia ya Waluguru na kwa kufanya hivyo nchi itaendelea kutunza utamaduni wake kupitia makabila machache yanayoendelea kutunza mila na utamaduni wao.


“lakini naomba msiende kuviweka ndani ili historia ya waluguru isife kwa sababu tunasema taifa lisilokuwa na utamaduni wake lisilokuwa na asili ni sawa na taifa ambalo halipo” alisema Bi. Regina.


Mkuu huyo wa Wilaya amesema kizazi cha sasa na kijacho kikijua mila na desturi za wazee wetu, vitu vilivyoheshimiwa, taratibu zilizokuwa zinafuatwa na mambo yaliyokuwa yanakatazwa kufanywa na makabila mbalimbali hapa nchini itasaidia kutunza maadili ya wanamorogoro na watanzania wote kwa jumla.


Akiongea katika tukio hilo la kukabidhiwa vifaa hivyo, Chifu Kingalu Mwanabanzi wa 15 kwanza amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuwaita Ofsini kwake kutambua vifaa hivyo vya mila na desturi vya kabila lao na kwamba vifaa hivyo vilipotea mwaka 1988 kwa kuibwa enzi za utawala wa chifu Kingalu Mwanabelege wa 12 aliyetawala kati ya mwaka 1954 hadi 1991.


Hata hivyo Chifu Kingalu Mwanabanzi wa 15 akipokea vifaa hivyo amesema mila ya Kabila la waluguru bado inafanya kazi na iko hai kwa maana ya kuwepo mawasiliano ya moja kwa moja kati yao na kile wanachokiamini hivyo hawako tayari kuvidharau vifaa hivyo vya kimila na kuahidi kuvirudisha katika himaya ya kichifu.


Naye Mlezi na mshauri  wa Shirika la wazee wa Mila na Desturi Mkoa wa Morogoro Bw. Mlenge Pakalapakala, amesema ataendelea kushirikiana na wazee hao na kutoa ushauri ufaao kwao ili kurudisha maadili ndani ya jamii ambayo yameonekana kuendelea kuporomoka kila kukicha kwa sababu ya jamii kudharau mila na desturi za wahenga wetu.



Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.