• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DED KILOSA APEWA SIKU 13 KUWAPATIA MAJI WAKAZI WA RUAHA

Posted on: September 17th, 2019

DED Kilosa apewa siku 13 kuwapa maji wananchi wa Ruaha

Na Andrew Chimesela – Ruaha, Morogoro

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa ametoa wiki mbili kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kuhakikisha anawapatia maji safi na salama wananchi wa Kata ya Ruaha iliyopo katika Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Waziri Majaliwa ametoa agizo hilo leo Septemba 17 alipokuwa anaongea na wananchi wa Kata ya Ruaha wakati wa ziara yake ya siku nne Mkoani Morogoro akiwa njiani kuanza ziara ya  siku moja Wilayani Kilosa kwa ajili ya kukagua  utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Wilaya hiyo.

Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya kibaoni akitoa taarifa ya kituo hicho kwa Mhe. Waziri Mkuu

Akianza ziara Wilayani humo, Waziri Mkuu alipokea kero ya maji kutoka kwa wananchi wa kata ya Ruaha kwamba ni ya muda mrefu. Mhe. Waziri Awali Waziri Mkuu alitaka kujua kutoka kwa Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Kilosa Joshi Chumu namna walivyolishughulikia suala hilo na gharama inayotumika katika kuchimba kisima kifupi cha maji.

Mhandisi Chumu alimueleza Waziri Mkuu kuwa uchimbaji wa kisima kifupi cha maji hadi kukamilika kwake kinagharimu kiasi cha shilingi milioni 30 na kwamba kazi hiyo inachukua siku mbili hadi kukamilika kwake.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt.Stephen Kebwe akitoa akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi wa Kibaoni Ifakara

Aidha, Waziri Mkuu alitaka pia kujua kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale kiasi cha fedha zilizopo sasa katika Halmashauri yake ambazo zinazotokana na  makusanyo ya ndani ya Halmashauri na kuambiwa fedha zililizopo hadi muda huo zilikuwa shilingi milioni 70.

Waziri Mkuu akianfgalia maelezo na mipango ya Upanuzi wa kiwanda cha Sukari cha Kilombero alipotembelea leo Septemba 17

Baada ya maelezo hayo kutoka kwa viongozi hao Mhe Waziri Mkuu akatoa agizo kutumia fedha hizo zote kwa maana ya shilingi milioni 70 zilizopo sasa, zitumike kuchimba visima vifupi vya maji kwa lengo la kuwapatia maji safi na salama wananchi wa kata ya Ruaha kama ufumbuzi wa kero hiyo ya maji kwa muda mfupi na kazi hiyo ikamilike kabla au ifikapo Septemba 30 mwaka huu.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiongea na wananchi wa Kata ya Ruaha Wilayani Kilosa

Kabla ya kufika eneo la Ruaha leo hii Waziri Mkuu alikuwa amekwishatembelea kituo cha Afya cha Kibaoni katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara na Kiwanda cha Sukari cha Kilombero. Kesho Septemba 18 Mhe Waziri Mkuu anatarajia kukamilisha ziara yake Mkoani Morogoro kwa kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro DC.

Ni sehemu ya wakazi wa Ruaha wakimsikiliza Waziri Mkuu

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.