• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Dk. Kebwe aagiza NIDA Kusogeza Huduma karibu na wananchi.

Posted on: August 22nd, 2019

Na. Andrew Chimesela -  Morogoro.


 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen kebwe ameutaka Uongozi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA  Mkoani humo kuongeza Idadi na kusogeza karibu na wananchi vituo vya kusajili wananchi ili kongeza kasi ya utoaji  namba na vitambulisho vya Taifa.


Dkt. Kebwe ametoa agizo hilo Kauli hiyo Agost 21, mwaka huu alipofanya ziara ya kushtukiza katika Ofisi za NIDA Mkoani humo zilizopo eneo la Tungi nje kidogo na Manispaa ya Morogoro kwa lengo la kujionea kasi ya utendaji kazi kulingana na muda uliobaki wa kukamilisha zoezi la kusajili kadi za simu kwa kutumia kitambulisho cha Taifa.


Akitoa maagizo kwa Viongozi wa NIDA Ofisini hapo, Mkuu wa Mkoa amewataka kusogeza karibu huduma hiyo kwa wananchi hasa kwa kuzingatia bado idadi kubwa ya wakazi wa Morogoro hawajasajiliwa kutokana na kituo cha NIDA kuwa kimoja.


“Natoa maagizo kwenu viongozi muhakikishe mnafungua Ofisi nyingine eneo  la mjini ili kusogeza karibu huduma kwa wananchi, yapo majengo ambayo mnaweza kuyatumia kwa sasa kama pale stendi ya Msamvu na jengo la zilizokuwa Ofisi za Halmashauri ya Morogoro vijijini”,

Alisema.


Dkt. Kebwe. ameitaka Mamlaka hiyo kumpa taarifa endapo kuna sehemu inahitaji msaada kutoka Uongozi wa Mkoa ili kuhakikisha shughuli za usajili zinakamilika kwa wakati.


Sambamba na hayo Dkt. Kebwe amewataka wataalamu wa NIDA kuongeza kasi ya utendaji kazi hususan katika zoezi la utoaji namba za vitambulisho ili kuwarahisishia wananchi kukamilisha mahitaji yao mbalimbali ikiwemo usajili wa namba za simu.


Amesema zipo Halmashauri Mkoani humo ambazo zoezi hilo linakwenda vyema lakini akasisitiza kuongeza juhudi kwa baadhi ya Halmashauri ambazo utekelezaji wake wa zoezi hilo si wa kuridhisha ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijni.


Kuhusu sualala utoaji Elimu kwa wananchi juu ya zoezi hilo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ameitaka NIDA Mkoani humo kushirikiana na vyombo vya habari vilivyopo ndani ya Manispaa ya Morogoro ili kufikisha elimu kwa wananchi walio wengi.


Pamoja na hayo Mkuu wa Mkoa ameyataka makampuni ya mawasiliano ambayo hayajaweka vituo vyake vya kusajili laini za simu nje ya jengo la Ofsi za NIDA Mkoani humo kuhakikisha  wanaweka vituo hivyo lengo likiwa ni kumwezesha mwananchi kupata huduma ya kusajili namba zao za simu punde tu anapopata kitambulisho chake cha Taifa.


Kwa upande wake Afisa Msajili Mfawidhi wa NIDA Mkoa wa Morogoro James Malimo amesema wamepokea maagizo ya Mkuu wa Mkoa na watayatekeleza huku akiahidi kuwa kufikia Jumatatu ya tarehe 26 mwezi huu watafungua kituo kingine katika maeneo jirani na wananchi ikiwemo katika jengo la zilizokuwa Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kama walivyoelekezwa na Kiongozi wao.


Amesema katika zoezi hilo la Usajili tayari asilimia 90 ya wakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wameshasajiriwa huku waliopata namba za vitambulisho ni asilimia 75.


Mwezi Aprili mwaka huu akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Mbeya, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliitaka Mamlaka ya Mawasiliano Nchini TCRA kutowabugudhi wananchi ambao hawatoweza kusajili laini zao za simu hadi kufikia mwezi Mei na kuagiza zoezi hilo lisogezwe mbele hadi mwezi Disemba mwaka huu kutokana na Watanzania walio wengi kutokuwa na vitambulisho vya Taifa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.