• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Dkt. Kebwe watuliza Wakazi Mindu

Posted on: February 21st, 2019

Kebwe awatuliza Wakazi  Mindu

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe amewatoa hofu  wananchi wa Kata ya mindu wanaoishi karibu na Bwawa la Mindu kwa kuwataka wawe watulivu wakisubiri maelekezo kutoka Serikalini kuhusu changamoto inayojitokeza katika eneo wanaloishi.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo jana Februari 20, 2019 wakati anazaungumza na wananchi wa Mitaa mitatu ya Kata ya Mindu wanaokaa karibu na Bwawa hilo kwa lengo la kuwafikishia ujumbe Mawaziri Nane waliotembelea Bwawa hilo hivi karibuni na kuangalia changamoto ya sheria ya mita 60 na mita 500 kwa wakazi na shughuli za kibinadamu zinaendeshwa jirani na bwawa hilo.

Katika ziara hiyo ambapo wakazi wengi walionekana kupatwa na mshtuko wakidhani Mkuu huyo wa Mkoa amepeleka ujumbe tofauti na ule uliotolewa na timu ya Mawaziri Nane waliofika katika bwawa hilo hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa aliwatoa hofu kuwa yeye hana jambo jingine jipya.

“Kwa hiyo tumeona tuje tuwatoe hofu wananchi kuhusu hili wala hakuna jambo jingine lolote lile” alisema Dkt. Kebwe

Hata hivyo Dkt. Kebwe aliwatahadharisha wananchi hao kutojimilikisha maeneo katika eneo hilo wala kudanganywa na mtu au watu kwa kuuziwa viwanja katika eneo hilo ambalo maamuzi yake yanasubiriwa kutolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.

“Hili liko mikononi mwa Mwenye nchi, asije akatokea mtu akawaambia jamani hapa kuna kipande cha shilingi laki moja au shilingi laki mbili, tujihadhari kwa hilo” aliongeza Dkt. Kebwe

Awali timu ya Mawaziri Nane ikiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi  ilitembelea Bwawa hilo na ikatoa maelekezo kwa Mkoa kusimamisha programu yoyote inayoendelea  katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na ile ya kutaka kuwahamisha wakazi wa eneo hilo hadi hapo watakapopewa  maelekezo kutoka Serikalini huku ikiwataka pia kuzuia watu wasiendelee kuongezeka katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa Ofisa wa Bodi wa Bonde la Wami Saimoni Ngonyani alibainisha kuwa Bwawa la Mindu ambalo linachangia kwa asilimia 80 ya upatikanaji wa maji kwa wakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro limekubwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupungua kwa kina kunakosababishwa na shughuli za kibinadamu zinazofanyika katika maeneo ya karibu na bwawa hilo.

Afisa Habari

RS Morogoro

20 Februari, 2019

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.