• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Jafo atoa mwezi mmoja ujenzi wa kituo cha Afya mikumi

Posted on: January 2nd, 2019


Na Andrew Chimesela – Morogoro,

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh. Selemani Jafo ametoa mwezi mmoja kwa uongozi wa Wilaya ya Kilosa kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mikumi baada ya kuonekana kasi ya ujenzi huo kusuasua.


Waziri Jafo ametoa agizo hilo Januari 2 mwaka huu alipofanya ziara ya siku moja wilayani Kilosa Moani Morogoro ambapo ametembelea ujenzi wa kituo cha Afya cha Mikumi, mto Ruhembe unaolalamikiwa na wananchi kupoteza maisha ya watu hususan kipindi cha masika na kuhitimisha ziara hiyo kwa kutembele Kituo cha Afya cha Kidodi.


Amesema fedha za Ujenzi wa Kituo hicho cha Afya Mikumi zilipelekwa mwishoni mwa mwezi Juni 2018 na ujenzi wake ulitakiwa kukamilika mwezi Novemba, 2018 hata hivyo ujenzi huo hadi sasa bado unasuasua hivyo kutoa mwezi mmoja kwa uongozi hadi Januari 30 mwaka huu ujenzi huo uwe umekamilika.


“lakini vile vile barua ni jambo la kwanza ninyi pale mmechelewa sana itakapofika tarehe thelathini mwezi wa kwanza nikute majengo yote yale yawe yamekamilika, kuta zimepandishwa kila kitu nitakuja mwenyewe kukagua majengo yale” amesema Waziri Jafo.


Katika hatua nyingine Waziri jafo amepongeza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kidodi kwa kuwa ujenzi wake umekamilika kwa wakati ingawa bado kuna mapungufu madogo ya kumalizia na akaagiza kukamilisha mapungufu hayo ifikapo Januari 15 mwaka huu.

Kwa upande wa ujenzi wa daraja la mto Ruhembe ambao upo Tarafa ya Mikumi unaolalamikiwa na wananchi wa eneo hilo kusababisha vifo vya watu unapojaa maji hasa kipindi cha masika Waziri huyo ameahidi kulibeba suala hilo kwa uzito na kwamba ataangalia namna ya kulifanyia kazi ili kutatua changamoto hiyo.

Katika ziara hiyo Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe. Joseph Haule amemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya na akatumia fursa hiyo kuiomba serikali iendelee kusaidia Jimbo la Mikumi na Wilaya ya Kilosa kwa Jumla hususan sekta ya Afya.



Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.