• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA SIASA MKOA WA MOROGORO YAWAFARIJI WAHANGA WA MAFURIKO

Posted on: February 7th, 2020

KAMATI YA SIASA MOROGORO WAWAFARIJI WAHANGA WA MAFURIKO

Na Andrew Chimesela


Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Morogoro, wamewatembelea na kuwafariji kwa kutoa misaada kwa wahanga wa mafuriko yaliyotokea katika Kijiji cha Dakawa Wilayani Mvomero yaliyotokanana na Mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini.

Wajumbe wa Kamati hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wake Innocent Kalogeresi wamewatembelea wahanga hao Februari 7 mwaka huu baada ya kukatisha kwa muda ziara yao ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayoteklelezwa ndani ya Mkoa huo.

Baada ya kufika eneo la tukio, Mwenyekiti Innocent Kalogeresi amewapa pole wananchi waliopatwa na kadhia hiyo huku akiwataka wananchi ambao bado wako maeneo ya mabondeni ambayo ni hatarishi kuondoka kwenye maeneo hayo ili kunusuru maisha yao.

“ombi langu pengine kwa namna moja ama nyingine wapo ndugu rafiki ambao bado wanang’ang’ania kuwa kule waambieni waje mahali ambapo pako salama, mto wami una mamba wengi pengine kuendelea kubaki kule tunaweza kupata ajali nyingine ambayo haina sababu” ameonya Kalogeresi

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewataka wananchi ambao nyumba zao zimezingirwa na maji kutorudi haraka kwenye makazi yao  kwani amesema nyumba hizo zinaweza kuanguka kwa sababu ya kuta zake kulowa maji na kusababisha madhara makubwa kuliko ya sasa.

.Kwa sababu hiyo, Mhandisi Kalobelo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amesema ataunda timu ya wataalamu kwenda eneo la tukio na kufanya tathmini ya kina ili kujua usalama wa nyumba zilizolowa maji  na kutoa taarifa kwa wenye nyumba hizo kama wanaweza kurudi katika makazi yao ama la, kwa lengo tu la kulinda na kuokoa maisha yao.

“tahadhari yangu, tusiingie haraka haraka kwenye nyumba hizi ambazo zimeingiwa na maji ili tujihakikishie  usalama wake” alishauri Mhandisi Kalobelo


Pamoja na ushauri wa pande hizo mbili, Kamati hiyo ya siasa baada ya kuguswa na tukio hilo imekabidhi msaada wa chakula na misaada mingine kwa wahanga waliokuwa kwenye Kambi iliyokuwa imeandaliwa na Serikali ngazi ya Wilaya kushirikiana na Mkoa.

Misaada iliyotolewa ni pamoja na mchele, unga wa ngano, unga wa sembe, mafuta ya kula pamoja na maharagwe huku Katibu Tawala wa Mkoa akitoa wito kwa taasisi zote za Serikali na binafsi ndani ya Mkoa huo kushirikiana pamoja kuwasaidia wahanga waliopatwa na mafuriko hayo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Florent Kyombo, amesema kaya 355 zenye jumla ya wananchi zaidi ya 800 zimeathirika na mafuriko hayo yaliyotokana na mvua zilizonyesha mikoa ya kaskazini hususan Mkoa wa Manyara usiku wa kuamkia Februari 6 mwaka huu na maji yake kuathiri eneo hilo la Kijiji cha Dakawa.

Kamati ya siasa iliendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Kilosa, ambapo pamoja na miradi mingine ilitembelea mradi wa ukarabati wa shule ya Sekondari ya Kilosa na baadae ikawasili Wilayani Gairo.

hili ni moja ya majengo ya shule ya Sekondari ya Kilosa yaliyokarabatiwa.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • RC SANARE: NENDENI MKAJIFUNZE MALINYI.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.