• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU ASIFU TARURA – IFAKARA.

Posted on: July 25th, 2018

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU ASIFU TARURA – IFAKARA
Na. Andrew Chimesela - Ifakara
Ikiwa ni siku ya tano tangu Mwenge wa Uhuru kuanza kukimbizwa Mkoani Morogoro leo umekimbizwa katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara na kutembelea miradi saba yenye jumla ya thamani ya shilingi 1.9 Bil. ukiwemo Mradi wa Barabara ya Upogolo yenye urefu wa 1.3 Km.
Baada ya kutembelea Barabara hiyo Kiongozi wa Mbioza Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Kabeho amesifu utendaji kazi wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini - TARURA kutoka katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara kutokana na kile alichoita kazi hiyo kinafanana na thamani ya fedha zilizotumika 
Charles Kabeho amewamwagia sifa watendaji hao wa TARURA Halmashauri ya Mji Ifakara Julai 25 mwaka huu wakati wa Mbio za Mwenge wa uhuru uliokimbizewa ukitokea katika Halmashauri ya Morogoro DC na kuanza kukimbizwa Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro.

Awali Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge alipofika katika Barabara hiyo alianza kumuuliza maswali mbalimbali Meneja wa TARURA wa Halmashauri ya Ifakara na kupewa majibu ambayo yalimfanya kupima upana wa barabara hiyo inayojengwa kwa kiwango cha Changarawe hivyo kutoa tape measure kutoka mfukoni mwaka na kuanza kupima.

Aidha, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru hakuishia hapo alimtaka Meneja huyo, Waandishi wa Habari pamoja na viongozi wengine wa ngazi ya Wilaya akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo kupanda kwenye magari ili kupima urefu wa barabara hiyo kwa lengo la kujiridhisha kama barabara hiyo ina urefu uliotajwa kwenye taarifa.

Baada ya kukamilika kwa mtihani huo majibu yalitolewa kuwa yanafanana na maelezo yaliyotolewa katika taarifa iliyosomwa kwake awali, jambo lililomsukuma kuwapongeza Viongozi wa TARURA wa Halmashauri hiyo ya Ifakara kwa kusema ukweli na kufanya kazi kulingana na mikataba inavyoelekeza.

“kwanza ninachoweza kuwashauri watendaji wote wanaotekeleza miradi ya maendeleo, wawe wanazingatia viwango vinavyotajwa kwenye mikataba. Lakini pia wasisite kuchukua hatua pale ambapo Mkandarasi anafanya kazi tofauti na mikataba hiyo.alisema Charles Kabeho.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo alimsifu Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge Kitaifa mwaka 2018 kuwa yupo imara na kumuomba aendelee kusimamie suala zima la mlinganyo kati ya fedha na kazi (Value for money) ili fedha zinazotolewa na Serikali zilete matunda kwa Jamii.

Awali akisoma taarifa ya Mradi huo wa barabara ya Upogolo itakayogharimu zaidi ya shilingi 400 Mil. hadi kukamilika kwake, Meneja wa TARURA Halmashauri ya Mji wa Ifakara Imannuel Mfinanga, alisema eneo la Upogolo lina changamoto ya kujaa maji kipindi cha masika hivyo mradi huo wa barabara unalenga kuondoa changamoto hiyo na kuwawezesha wananchi kupata huduma za mahakama na Kituo cha Polisi kwa kipindi chote cha mwaka.
MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.