• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

madiwani ulanga waaswa

Posted on: May 20th, 2020

Madiwani watakiwa kuhamasisha ukusanyaji mapato

 

Na Andrew Chimesela,  Morogoro

Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga limeaswa kuwa na utamaduduni wa kuwahamasisha wananchi wa maeneo yao katika suala nzima la kulipa kodi na michango mingine halali ili kuongeza mapato ya halmashauri hiyo na kusaidia kuleta maendeleo yao.

Rai hiyo imetolewa Mei 19 mwaka huu Wilayani Ulanga na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati wa Baraza Maalum la madiwani la Halmashauri hiyo wakati wa kujadili taarifa na majibu ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Amesema Waheshimiwa madiwani wanalazimika kuwa mfano na kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha wananchi kwenye maeneo yao kuelewa faida ya ukusanyaji wa kodi ili waweze kutoa kodi kwa maendeleo yao badala ya madiwani hao kuwahamasisha wananchi hao kutolipa kodi au  tozo mbalimbali.

“Maeneo mengine madiwani wengine ndio shida, wanahamasisha wananchi wavunje utaraibu, wanahamasisha wananchi wasilipe kodi, hii ni shida sana na kwa bahati mbaya sana tunazo taarifa za madiwani wa Kata hizo wanaofanya mambo kama hayo hatutawavumilia” ameonya Loata Sanare.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare akiongoza Kikao cha Baraza Maalum katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga Jonas Mallosa kufuata taratibu zote za ukusanyaji na utumiaji wa fedha zinazokusanywa kutoka vyanzo mbalimba vya mapato ya ndani kwamba fedha hizo zikusanywe kwa njia ya kielecktroniki na kisha kupelekwa benki kabla ya kuzitumia.

“Fedha zote Mkurugenzi hakikisha zinaingia benki kwa utaratibu wa elektroniki, hunyimwi kutoa na kutumia unavyotaka wewe, katika maeneo mengi ndani ya halmashauri zetu wanakata hela huko huko juu kwa juu wanawapatia shida vijana wale wanaotukusanyia fedha kwa sababu maelekezo yanatoka kwa Mkurugenzi, maelekezo yanatoka kwa DT maelekezo yanatoka kwa yule jamaa mwingine” amesema Loata Sanare.

DC Ulanga Ngollo Malenya akisikiliza kwa makini hoja zinazotolewa wakati wa Baraza maalum la Halmashauri hiyo, Mei 19 mwaka huu

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewaonya watumishi wa serikali Wilayani ambao hawatoi ushirikiano kwa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali kutoa ushirikiano unaohitajika kwa kiongozi huyo pindi inapohitajika ili kuleta ufanisi wa kazi yake na kuongeza maendeleo ya Halmashauri hiyo.

Kiongozi huyo ambaye ndiye mwenyekiti wa kikao hicho cha Baraza Maalum la Madiwani kwa ajili ya kutekeleza agizo la Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI amesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watumishi hasa wakuu wa Idara, kusababisha kuendelea kwa Hoja zisizo na majibu suala ambalo linaharibu taswira ya utendaji wao na Mkoa kwa jumla.

Baadhi ya wajumbe na waalikwa wa kikao hicho cha Baraza

Katika kikao hicho cha Baraza Maalumu, mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za serikali Mkoa wa Morogoro, ameeleza kuwa pamoja na Halmashauri ya wilaya ya Ulanga kupata hati inayoridhisha, bado kuna hoja tano zilizokosa majibu.

Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Morogoro CPA Peter Mwabwanga


Miongoni mwa hoja zinazoelezwa kukosa majibu, ni pamoja na Usimamizi wa watumishi, baadhi ya taarifa za manunuzi, taarifa za mikataba mbalimbali toka ofisi ya mwanasheria pamoja na kutozingatiwa kwa baadhi ya maagizo ya serikali.

Makamu Mw wa Baraza la Halmashauri ya Ulanga

 

Viongozi wa Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.