• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MAJALIWA ARIDHISHWA NA UJENZI WA SGR

Posted on: May 14th, 2020

MAJALIWA ARIDHISHWA NA UJENZI - SGR

Na Andrew Chimesela – Morogoro

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ameonesha kuridhishwa na ujenzi wa mradi wa reli ya mwendo kasi (Standard Gauge Railway – SGR) unaotekelezwa kuanzia kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro hususan ujenzi wa handaki lenye urefu wa kilometa moja linalojengwa Wilayani Kilosa ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 83.

Waziri Mkuu akiwasili kwa Helkopta eneo ambalo handaki limechorongwa kwa ajili ya kupita reli ya SGR, Kilosa Mkoani Morogoro

Waziri Mkuu amesema hayo Mei 14 mwaka huu baada ya kukagua kipande cha mradi huo na kuhitimisha ziara yake kwa kutembelea ujenzi wa handaki hilo lililochorongwa chini ya mlima nje kidogo ya Mji wa Kilosa ili kupitisha Reli ya SGR lengo likiwa ni kukwepa changamoto za mto Mkondoa ambazo mara kadhaa zimekuwa tishio kwa usafiri wa Reli katika eneo hilo.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (wa pili kulia), akiwa amepokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare (wa tatu kulia) wakati amewasili Wilayani Kilosa kwa ajili ya kutembelea handaki ambapo reli ya mwendo kasi itapita

Mhe. Kassim Majalwa akiwa ndani ya handaki

Katika hotuba yake fupi aliyoitoa mara baada ya kukagua handaki hilo Mhe. Majaliwa amesema ameridhishwa na ubora, kasi, na hatua iliyofikiwa ya Ujenzi wote wa SGR lakini pia kuridhishwa na kazi kubwa iliyofanywa ndani ya handaki hilo na kuwapongeza Kampuni ya Yarp Merkez iliyochaguliwa kutekeleza mradi huo, Wizara na watendaji wake wote.

Hili ndilo handaki lenye urefu wa zaidi ya 1Km linavyoonekana kwa ndani, ambalo Reli ya mwendo kasi itapita kutoka upande mmoja wa mlima kwenda upande wa pili  ili kuivusha reli hiyo kwenye mto Mkondoa. 



Handaki livyoonekana kwa nje

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewasihi watanzania waliopata kazi katika kampuni ya Yarp Merkez inayojenga reli hiyo kuongeza nguvu katika kufanya kazi  ili kukamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa. 

Akizungumzia faida ya reli hiyo Waziri Mkuu amesema mradi huo ni moja ya miradi ya kimkakati utakaokuza uchumi wa nchi lakini pia utaondoa changamoto ya ajira hususan vijana ambapo awali vijana wengi walikuwa wakikaa vijiweni lakini kupitia mradi huo na mradi wa Bwawa la Mwl. Nyerere juma ya vijana elfu 18 wameajiriwa.

 

Waziri Mkuu akipewa maelezo na Watendaji wa TRC kuhusu ujenzi wa handaki hilo.

Aidha, Waziri Mkuu amesema reli hiyo itakapokamilika itafanya kazi masaa yote kwa kuwa itaendeshwa kwa umeme utakaounganishwa kutoka katika vyanzo vitatu vya uhakika ukiwemo ule unaotoka Bwawa la mwalimu Nyerere, umeme wa Kidatu unaozarishwa kutokana na bwawa la Mtera na umeme wa Kinyerezi unaotokana na gesi hivyo Reli hiyo haisimama kufanya kazi kwa sababu ya kukosa nishati ya umeme.

Ili kuwahakikishia zaidi watanzania Waziri Mkuu amesema, endapo vyanzo vyote hivyo vya umeme umeme wake ukikatika jambo ambalo ni nadra kutokea, bado reli hiyo itaendelea kufanya kazi kwa kutumia mtambo maalum utakaokuwa umefungwa kwenye reli yenyewe ukiwa na uwezo wa kuendesha reli kwa dakika 45.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (katikati) akiwa na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare (kulia) wakati wa kutembelea handaki la SGR nje kidogo ya Mji wa Kilosa

Akitoa rai kwa watanzania waliopata ajira kwenye mradi huo Majaliwa  amewataka kutumia fursa hiyo kwa kujenga uaminifu na kujituma huku akiwataka kujituma kupata ujuzi katika sekta walizopo ili baadae waweze kujiajiri ama kuajiri vijana wengine pamoja na kuomba tenda katika miradi mbalimbali.

Akizungumzia suala la ugonjwa wa CORONA, Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare kutoa maelekezo kwa Wakuu wa Wilaya katika Mkoa huo kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi juu ya ugonjwa huo namna unavyoenea na namna ya kujikinga kwa kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa Afya lakini amewataka wafanye hayo  wakiendelea na kufanya shughuli zao za kila siku.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa ndani ya Helkopta tayari kwa safari ya kurudi Dodoma

Mradi wa Reli ya mwendo kasi ambao umeelezwa kuwa utawanufaisha watanzania kwa kipindi cha miaka 100 ijayo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Juni mwakani.

 

mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • NIMR YAANZA TAFITI ZA KUTIBU MALARIA.

    January 22, 2021
  • RC Morogoro atoa siku 11.

    January 21, 2021
  • WANACHI KIJIJI CHA WAMI LUHINDO WAHAMASIKA KUJENGA SHULE, WAOMBA SIKU YA HARAMBEE IPANGWE KARIBU.

    January 17, 2021
  • Miradi 67 ya maji kutekelezwa Morogoro.

    January 15, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.