• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mkimbiza Mwenge Kitaifa akataa kukabidhi Hati Miliki za Kimila 250.

Posted on: July 25th, 2018

Mkimbiza Mwenge Kitaifa akataa kukabidhi Hati Miliki za Kimila 250
Na. Andrew Chimesela - Morogoro
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa mwaka 2018 ndugu Charles Kabeho amekataa kukabidhi hati miliki za kimila 250 kwa wananchi wa Kijiji cha Mikese ambacho kipo ndani ya mradi wa Upimaji na Urasimishaji wa Ardhi unaofanyika chini ya Shirika la PELUM Tanzania kwa madai ya taarifa za kifedha za mradi huo zina zina kasoro.

Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge amekataa kukabidhi hati hizo Julai, 24 mwaka huu wakati wa kukimbiza Mwenge wa Uhuru ambao ulikimbizwa katika Kijiji cha Mikese ambapo ratiba ilionesha Kiongozi huyo kutakiwa kukabidhi hati hizo 250 za wananchi wa Kijiji hicho kati ya Hati miliki 750 ambazo ziko tayari kutoka vijiji vingine vya Kata ya Mikese.

Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge Kitaifa alieleza sababu ya kutokabidhi hati hizo kuwa kulikuwa na mapungufu katika utoaji wa gharama zilizotumika kwenye mradi huo huku akibainisha kuwa taarifa zilizoandaliwa na Mkoa huo zinasema gharama ya mradi wa Upimaji na Urasimishaji Ardhi zilizotumika ni shilingi 100 Mil. wakati taarifa za kutoka Halmashauri ya Morogoro zinaonesha gharama gharama zilizotumika ni shilingi 153, 120,000/=

“Mradi wa Upimaji na Urasimisha wa Ardhi kwa Wananchi, taarifa zake za fedha zimekuwa tofauti, Kitabu cha Mkoa kinasema shilingi milioni 100 lakini taarifa husika inasema shilingi 153,120,000/= ongezeko la shilingi 53,120,000/= ni fedha ambazo ni nyingi” alisema Kiongozi huyo.
Amesema Mradi huo ni wa fedha za wahisani zimetolewa ili kuondoa migogoro ya ardhi iliyokithiri Mkoani Morogoro, hivyo sio vema kuacha suala hilo kirahisi huku lina kasoro zinazoonesha kuwa ni za ubadhirifu huku kukiwa na tofauti ya kiasi kikubwa cha fedha.

Kwa sababu hiyo Ndugu Charles Kabeho ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuuchunguza mradi huo ili kupata ukweli wake huku akizitaka hati zote zilizotakiwa kukabidhiwa kwa wananchi zisitolewe kwa wananchi husika zihifadhiwe Ofisi ya Usalama ya Mkoa kwa usalama zaidi hadi uchunguzi wa suala hilo utakapokamilika.

Pamoja na maagizo hayo, Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge Kitaifa, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro kusimamia suala hilo kwa karibu na endapo uchunguzi utabaini ubadhilifu wa aina yoyote, basi wahusika wote wa sakata hilo wachukuliwe hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.

Akijibu mkanganyiko huo ulivyotokea baada ya kuulizwa swali na Mkimbiza Mwenge Kitaifa, Mratibu wa mbio za Mwenge Kimkoa Mkoa wa Morogoro Bw. Diazi Ndomba amesema taarifa ambayo ipo katika kitabu cha miradi ya Mwenge ya Mkoa huo ililetwa na Halmashauri husika na wao ndio wanaweza kutoa maelezo ya kina kuhusu utofauti huo.

Naye Mratibu wa shirika la PELUM Tanzania Bw. Anglolile Reyson amesema mchakato wote kuhusu suala la Upimaji na Urasimishaji wa Ardhi kwa wananchi wa vijiji vinavyohusika na mradi huo umefuata taratibu zote zinazotakiwa.
Mradi wa Upimaji na Urasimishaji Ardhi kwa wananchi umefanyika katika Kata ya Mikese, na kuhusisha Vijiji vya Mikese, Newland, Lubungo na Mfumbwe. Jumla ya Hati Miliki za kimila 750 zimeandaliwa kutolewa kwa wananchi wa Vijiji vya Mikese hati 250, Newland hati 160, Lubungo hati 175 na Mfumbwe hati 165.
MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.