• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro yapongezwa utekelezaji wa Miradi Mkakati

Posted on: February 23rd, 2019

Morogoro yaongoza kufanya vema miradi ya Kimkakati, viongozi  wapongezwa.

Na Andrew Chimesela - Morogoro

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ameupongeza Uongozi wa Mkoa wa Morogoro kwa kutekeleza vizuri ujenzi wa Soko Kuu linalojengwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Waziri Jafo ametoa pongezi hizo jana Febr. 23 alipotembelea Ujenzi wa miradi mbalimbali Mkoani humo ikiwa ni pamoja na miundombinu inayojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mvomero, jengo la akina mama na baadae kutembelea ujenzi wa Soko Kuu linalojengwa mjini Morogoro.

Waziri Jafo alionesha kuridhika na kasi pamoja na ubora wa ujenzi huo huku akisema kati ya miradi yote ya Kimkakati  inayotekelezwa hapa nchini ni mradi wa soko hilo Mkoani Morogoro pekee ndiyo iliyofanya vizuri katika utekelezaji wake hivyo akawapongeza Viongozi wa Mkoa huo wakingozwa na Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Kebwe Stephen Kebwe kwa kusimamia vizuri ujenzi huo.

Amesema, kwa kazi nzuri inayofanywa na Halmashauri hiyo, yuko tayari kupitisha fedha za miradi mingine ya aina hiyo iwapo wataomba. “kwa speed hii inayoendelea sio dhambi watu kama ninyi kuwapa mradi mwingine, sio dhambi” alisisitiza Mhe. Jafo.

Akiwa Wilayani Mvomero pamoja na kupongeza kazi inayoendelea katika ujenzi wa majengo mengine ya Hospitali ya Wilaya hiyo, Waziri Jafo aliwaonya watumishi wote hapa nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe pamoja na kupokea maelekezo yaliyotolewa na Waziri huyo mwenye dhamana ya TAMISEMI, alibainisha siri ya mafanikio ya ujenzi wa soko Kuu la Manispaa ya Morogoro kuwa ni ushirikiano mzuri uliopo baina ya viongozi wa ngazi zote.

Hata hivyo alimueleza Waziri wa TAMISEMI kuwa tayari kuna miradi ambayo imeshaanza kuibuliwa ukiwemo Mradi wa machinjio ambao umeibuliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa lengo hilo la kutaka kujitegemea kimapato.

Kwa upande wake Mstahiki meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga, pamoja na kutoa shukrani kwa Serikali ya Mhe. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha kwa ajili ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwemo Ujenzi wa vituo vya Afya, bado alimueleza Waziri juu changamoto iliyopo juu jengo la standi Kuu ya mabasi ya Msavu na kuomba ishughulikiwe.

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Waziri Mahiga awataka watanzania kutoa haki kwa watoto wao

    December 11, 2019
  • Walimu 400 sasa kutumia TEHAMA kufundishia

    November 30, 2019
  • Magereza Yarejesha Eneo kwa Wananchi Ifakara

    December 06, 2019
  • Waziri Kairuki ampongeza RC Sanare kutenga maeneo ya uwekezaji Morogoro.

    December 04, 2019
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2018 Mkoa wa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa