• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Rais Magufuli ataka mashamba yanayofutwa wapewe Wananchi Maskini

Posted on: June 29th, 2020

Magufuli ataka mashamba yanayofutwa wapewe wananchi maskini

Na Andrew Chimesela – Morogoro

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe  Magufuli ameuagiza uongozi wa Wilaya ya Kilosa na Mkoa wa Morogoro kwa jumla kupanga mikakati mathubuti ya kugawa mashamba yanayofutwa na Serikali kwa wananchi maskini ili kukomesha migogoro inayojitokeza Mkoani hapa.

Rais Magufuli ametoa agizo hili Juni 29, 2020 akiwa Wilayani Kilosa wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Mradi wa ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) sehemu ya Morogoro hadi Makutupora  na ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Rudewa hadi Kilosa yenye urefu wa Km 24.

Akitoa hotuba yake mbele ya maelfu ya wananchi wa kilosa na maeneo jirani, Rais Magufuli amesema sababu kubwa ya migogoro ya ardhi inayojitokeza Mkoani Morogoro inatokana na mashamba makubwa kuchukuliwa na matajiri.

Kwa sababu hiyo pamoja na mashamba 49 aliyokwisha yafuta, bado amemuagiza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kabla ya jumamosi ya wiki hii, kumpelekea taarifa ya mashamba mengine 11 ili ayafute na kuwagawaia wananchi Maskini lengo ikiwa ni kukomesha Migogoro hiyo.

“lakini ninachotaka kifanyike, na hili ni la muhim zaidi, uongozi wa Wilaya ya Kilosa, na uongozi wa Wilaya zote katika Mkoa wa Morogoro, wakae, haya mashamba yaliyofutwa ni lazima tuyagawe bure kwa wananchi maskini” aliagiza Rais Magufuli.

Amesema, imekuwa ni kawaida mashamba hayo yanayofutwa kugawana matajiri badala ya kutoa kwa maskini ambao ndio walengwa na kusababisha migogoro ya ardhi kuendelea kujitokeza Mkoani Morogoro, hivyo ameagiza  uwepo usimamizi madhubuti katika ugawaji wa mashamba yote yanayofutwa.

Akizungumzia Mradi wa ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) sehemu ya Dar es Salaam hadi Morogoro ambao umefikia asilimia 82, Rais Magufuli amefurahishwa na ujenzi huo hususan handaki alilolikagua lenye urefu wa zaidi ya Km 1, na kufurahishwa kuwa ujenzi wake umezingatia kiwango na kasi.

Kuhusu ujenzi wa Barabara ya kiwango cha lami ya kutoka Rudewa hadi Kilosa, inayojengwa na Wakandarasi wazawa, Dkt. Magufuli amesema hajaridhiswa na kasi ya ujenzi huo kwa kuwa ni wa kusuasua. Kwa sababu hiyo ametoa kipindi cha mwezi mmoja Wakandarasi hao kubadilika.

Amesema wasipobadilika atawanyang’anya kazi hiyo na kwamba kuanzia sasa Wakandarasi hao waanze kujenga barabara hiyo usiku na mchana. Amesema, wakandarasi wazawa wamekuwa wakilalamika kutopewa zabuni za kujenga barabara na miundombinu mingine lakini haipendezi wanapopewa zabuni hizo hawazitumii ipasavyo.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amemwagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi  na Mawasiliano Isack Kamwelwe kuanza kufanya Upembuzi yakinifu wa barabara ya kutoka Kilosa Mjini kwenda Mikumi (Km 78) ili itafutiwe fedha na kujengwa kwa kiwango cha lami.

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • NIMR YAANZA TAFITI ZA KUTIBU MALARIA.

    January 22, 2021
  • RC Morogoro atoa siku 11.

    January 21, 2021
  • WANACHI KIJIJI CHA WAMI LUHINDO WAHAMASIKA KUJENGA SHULE, WAOMBA SIKU YA HARAMBEE IPANGWE KARIBU.

    January 17, 2021
  • Miradi 67 ya maji kutekelezwa Morogoro.

    January 15, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.