• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO ATOA MWEZI MMOJA WANANCHI WA MALINYI KUPATA MAJI

Posted on: August 25th, 2020

RAS MOROGORO ATOA MWEZI MMOJA MALINYI KUPATA MAJI


Na Andrew Chimesela – Morogoro

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo ameagiza Wakala wa Usamabazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini - RUWASA Mkoani humo, kuhakikisha wananchi wa Malinyi wanapata huduma ya maji Safi na Salama ndani ya kipindi kisichozidi mwezi mmoja kuanzia Agosti 25 mwaka huu.

Mhandisi Kalobelo ametoa agizo hilo Agosti 25 mwaka huu, Wakati wa Kikao cha pamoja cha kujadili hatma ya Mradi wa Maji wa Malinyi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofsisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Agizo hilo limekuja baada ya mradi wa Maji wa Malinyi ulioanza kujengwa mwaka 2015 kutokamailika kutokana na changamoto zilizojitokeza wakati wa kusanifu Mradi, hivyo maji kushindwa kufika kwenye tenki.

Baada ya changamoto hiyo kujitokeza uongozi wa Mkoa wa Morogoro umeamua kuingilia kati na kuandaa kikao kwa kuwakutanisha Wadau wa Mradi huo ili kutafuta njia mwafaka ya kuwafikishia maji wananchi wa Malinyi.

Pamoja na kutafuta njia za kufanikisha mradi huo, wajumbe walikubaliana kuwa njia sahihi na ya haraka ya kuwapatia maji wananchi wa Malinyi na kuondokana na kero hiyo, ni kuchimba visima virefu. ndipo Mwenyekiti wa kikao hicho, ambaye pia ndiye Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo akatoa agizo.

“Mimi nisema watu wa Malinyi wanahitaji maji, yanatoka wapi is non of their business (sio kazi yao). Kwa hiyo RUWASA kama RUWASA Option hiyo ya kupeleka visima ichukueni walau kwanza watu wapate maji kwa muda mfupi inavyowezekana na ikiwezekana ndani ya mwezi huu wa tisa” aliagiza Mhandisi Kalobelo.

Hata hivyo alieleza kuwa yeye hatengui maelekezo ya Waziri wa Maji aliyoyatoa alipotembelea mradi huo wa kuboresha mradi wa Maji wa Malinyi bali aliwataka waendelee kuyatekeleza kama Waziri mwenye dhamana ya masuala ya Maji alivyoagiza.

“Maelekezo ya Waziri mimi sitaki kuyatengua. Maelekezo ya Waziri aliyeelekeza kwamba maboresho ya Mradi huu  yafanyike yatekelezwe.” Alisisitiza.

Aidha, Mhandisi Kalobelo amemtaka Mkurugenzi wa RUWASA kuwasiliana na watu Bonde ili kuhakiki ubora wa maji ya visima vinavyopedekezwa kuchimbwa ili mara visima vitakapokamilika maji yaingizwe kwenye miundombinu iliyokwishajengwa na wananchi waanze kupata huduma ya maji.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Kalobelo amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Morogoro - MORUWASA Mhandisi Tamim Katakweba kuhakikisha kazi ya kuboresha mradi wa awali inaendelea kufanyika na inakwenda sambamba na uchimbaji wa visima ambavyo vinatasaidia kuondoa tatizo la maji kwa haraka.

Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Mkoa wa Morogoro Mhandisi John Msengi ametoa wito kwa wananchi wa Malinyi kuendelee kuwa watulivu kwa kuwa Serikali kupitia uongozi ngazi ya Mkoa umeshatoa agizo kuwafikishia maji ndani ya mwezi mmoja.

Naye Mkandarasi wa Mradi wa Maji Malinyi Kambarage Masato kutoka Kampuni ya Aundacia Investment Ltd amesema amepokea maagizo ya Katibu Tawala wa Mkoa na kuahidi kuyatekeleza kwa wakati kama walivyokubaliana kwenye kikao hicho.

Kikao hicho cha kujadili hatma ya mradi wa maji Malinyi, kilijumuisha Wajumbe wa Menejimenti ya Mkoa wa Morogoro, Meneja wa RUWASA Morogoro, Mkurugenzi wa MORUWASA, Mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Malinyi na Mhandisi Mshauri wa Mradi huo.

Mradi wa Maji wa Malinyi ulianza kutekelezwa 26/92015, ambapo ulitakiwa kukamilika ndani ya miezi sita na baada ya kushindwa kukamilika ukaongezewa muda wa utekelezaji hadi 16/12/2017.

Mradi huu ulikuwa unatekelezwa na Mkandarasi Aundacia Investment Ltd chini ya Mkandarasi Mshauri wa Kampuni ya Interconsult. mradi ukikamilika unategemea kutoa huduma kwa watu zaidi ya elfu 17 wa vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makere.

Hadi sasa fedha zilizokwishalipwa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza mradi huo ni shilingi  2.9 Bil. sawa na asilimia 97.78 ya gharama yote ya ujenzi wa mradi huo ambao ni zaidi ya shilingi 3 Bil.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.