• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO APOKEA MICHANGO KUPAMBANA NA CORONA

Posted on: April 24th, 2020

RC Morogoro apokea  michango, awashukuru Wadau na kuwaasa.

Na. Andrew Chimesela, Morogoro.

Wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo wafanyabiashara Mkoani Morogoro wameanza kutekeleza ahadi zao za kutoa michango ya fedha na vifaa ili kusaidia kupambana na ugonjwa wa CORONA kama walivyoahidi Aprili 21 mwaka huu waliposhiriki kikao cha kujadili namna ya kupambana na ugonjwa huo Mkoani humo.

Wadau hao wameanza kutekeleza ahadi hiyo leo Aprili 24 kama walivyoahidi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare siku ya kikao  cha Aprili 21 mwaka huu na leo baadhi ya wadau hao wamefika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kutoa fedha na vifaa mbalimbali vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi 140Mil.


Mmoja wa wadau kutoka Islamic Foundation akikabidhi mchango wake kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro. Katikati anayeshuhudia ni Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo



Baadhi tu ya wadau wa maendeleo wakiwasilisha michango yao Kwa Mkuu wa Mkoa

Akiongea wakati wa tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare amewashukuru wadau wote walioamua kutoa michango yao ya fedha na vifaakinga mbalimbali kwa lengo la kusaidia juhudi za Mkuu huyo wa Mkoa na Serikali kwa ujumla katika kupambana na ugonjwa wa CORONA Mkoani humo.

Aidha, Loata Sanare amewahakikishia wadau waliotoa michango kuwa uadilifu mkubwa utazingatiwa katika kutumia fedha na vifaa vyote vilivyochangwa na vitakavyoendelea kuchangwa na kwamba vitatumika kama ilivyokusudiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare akimkabidhi Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Kusilye Ukio moja ya vifaa vilivyotolewa na wadau kwa ajili ya kupambana na ugonjwa wa CORONA. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wadau hao kutoa elimu kuhusu janga la ugonjwa wa CORONA kwa watu wanaowahudumia katika maeneo yao ya kazi au biashara zao na kuhakikisha wanawakinga na janga la ugonjwa huo.

“Na kikubwa sio fedha, kikubwa sio vifaa ambavyo mmevileta hapa, kikubwa ni kutoa elimu hii kwa watu ambo tunawahudumia” ameshauri Sanare

Lori la mizigo likiwa limebeba vifaa mbalimbali vya kusaidia kupambana na  maambukizi ya virusi vya COVID - 19 vilivyotolewa na wadau mbalimbali Mkoani Morogoro 

Tukio la kupokea michango hiyo ambalo ni la ahamu ya kwanza linalotarajiwa kuendelea kufanyika hapo kesho lilitanguliwa na ziara fupi ya Mkuu huyo wa Mkoa akiambatana na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na kutembelea kiwanda cha kushona nguo za michezo cha Mazava na kiwanda cha kutengeneza nguo cha 21st Centuary .

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa amewataka wamiliki wa viwanda hivyo kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa wa CORONA kwa kufuata maagizo yanayotolewa na Serikali na Wataalamu wa Afya ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wote kunawa maji tiririka kwa sabuni kila wanapoingia na kutoka kazini pamoja na kuwapima joto lao mara kwa mara ili kuepukana na maambukizi ya Virusi vya COVID - 19.

Mhe. Loata Sanare (katikati) na katibu Tawala wa Mkoa Mhandisi Emmanuel Kalobelo (kulia) wakiwa ghorofani wakiangalia wafanyakazi wa Kiwanda cha Mazava wakiwa kazini mara Mkuu wa Mkoa alipotembelea kiwanda hicho kilichopo katika Manispaa ya morogoro. Kushoto ni Meneja Uzalishaji wa kiwanda hicho Bw. Nelson Mchukye.

Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo alibainisha lengo la ziara ya Mkuu wa Mkoa kuwa ni kutaka kujionea uwezo wa Viwanda hivyo kama vinaweza kuzalisha kwa ubora unaohitajika vifaa vya aina yoyote vya kupambana na ugonjwa wa CORONA kama Barakoa,  lengo ni kutekeleza agizo la Rais  John Pombe Magufuli la kutengeneza vifaa hivyo hapa nchini.

Meneja Uzalishaji wa Kiwanda cha nguo cha Mazava Bw. Nelson Mchukya akimuonesha Mkuu wa Mkoa barakoa ambazo zimeanza kuzalishwa katika kiwanda hicho, ambapo Mkuu huyo wa Mkoa amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Ukio (mbele kushoto) kufuatilia barakoa hizo kama zina ubora unaostahili ili zitumike.

Kwa upande wao wadau waliofika kutoa michango, waliendelea kutoa ushauri kwa Serikali kuendelea kutoa elimu kwa jamii kujiepusha na mikusanyiko isiyo ya lazima lakini pia wakatoa wito kwa kila mmoja kwa Imani yake kumrudia Mungu wake ili kuliepusha taifa na janga hili hatari.

 

MWISHO

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.