• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro asitisha matumizi ya bweni la wanafunzi.

Posted on: November 12th, 2019


Na. Andrew Chimesela, Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare amesitisha matumizi ya  bweni la wavulana la shule ya msingi ya Berhnad Bendel iliyopo Manispaa ya Morogoro  kutokana na jengo hilo kukosa sifa ya kutumika kama bweni huku likihatarisha afya za wanafunzi.

Sanare amechukua uamuzi huo Novemba 11 mwaka huu alipotembelea shule hiyo iliyopo eneo la Kola na kushuhudia mazingira mabovu ya jengo hilo linalotumiwa na wanafunzi zaidi ya 100 ambapo aina ya ujenzi wake ukionekana kukosa sifa ya kutumika kama bweni huku likijengwa pasipo kufuata utaratibu wa ujenzi wa matumizi yenyewe.

Mazingira ya bweni hilo yalioneka kutopitisha hewa ya kutosha ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi wanaotumia huku ndani ya jengo kukitawaliwa na harufu kali inayotoka katika vyoo ambavyo vipo ndani ya jengo hilo.

Kutokana na hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ameagiza kusitishwa mara moja matumizi ya bweni hilo na kutaka wanafunzi hao watafutiwe sehemu nyingine iliyo salama watakayoitumia kama bweni mpaka hapo jengo hilo litakapofanyiwa marekebisho.

“kutokana na hali tuliyoiona wenyewe kwenye jengo lile, nasitisha kuanzia sasa lisitumike tena na muwatafutie sehemu nyingine salama wanafunzi hawa, lakini muhakikishe jengo hilo linajengwa upya ndani ya mwaka huu kwa kufuata utaratibu wa ujenzi wa bweni”, Alisema Sanare.

Hata baada kukosekana taarifa za ujenzi wa bweni hilo na  uhalali wa matumizi yake kama bweni Mkuu wa Mkoa Sanare amemuagiza Kamanda wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa  (TAKUKURU) Mkoa wa Morogoro Janeth Machulya kufuatilia taarifa ya ujenzi wa jengo hilo.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa  amemtaka Afisa Afya Mkoa wa Morogoro kuchukua hatua za kisheria kwa shule hiyo kufuatia kuwepo kwa mifereji ya maji taka inayotiririka kwenye maeneo yasiyo sahihi na kuhatarisha afya za wanafunzi.

Kuhusu ukaguzi wa mara kwa mara wa shule, Mkuu wa Mkoa amemtaka Mdhibiti ubora wa shule Manispaa ya Morogoro kuhakikisha anafanya zoezi la ukaguzi wa mara kwa mara ili kujiridhisha wakati wote mazingira ya shule yanakuwa safi na salama kwa wanafunzi na watumiaji wengine katika shule hiyo.

Kwa upande wake  Kamanda wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa  (TAKUKURU) Mkoa wa Morogoro Janeth Machulya amesema Taasisi yake imepokea maagizo ya Mkuu wa Mkoa na atayafanyia kazi mara moja.

Naye Mkuu wa shule hiyo SR. Levina August amekiri kuwepo kwa changamoto zilizoonekana katika ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa ambapo ameahidi kwasiliana na mmiliki wa shule hiyo ili kushughulikia maagizo yote yaliyotolewa na kiongozi huyo.

                                                                            MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.