• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro azindua zoezi la ugawaji vitambulisho

Posted on: May 21st, 2020

Viongozi tekelezeni wajibu, Maafisa Biashara tendeni haki – RC Sanare

Na Andrew Chimesela, Ifakara Morogoro

Viongozi mbalimbali wa Serikali Mkoa wa Morogoro wametakiwa kutimiza wajibu wao ipasavyo huku Maafisa Biashara ndani ya Mkoa huo kutakiwa kutenda haki wakati wote wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo 2020 ili nia njema ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwajali wanyonge iweze kutimia.

Rai hiyo imetolewa Mei 21 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati wa Uzinduzi rasmi wa ugawaji wa vitambulisho vya wafanya biashara na watoa huduma wadogo mwaka 2020 uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa iliyokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero Wilayani humo.

Loata Sanare amesema zoezi hilo ili mwaka huu litekelezwe kwa ufanisi,  ushirikiano thabiti unahitajika kuanzia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Ofisi za Wakurugezi Watendaji wa Halmashauri na Maafisa wa TRA huku Wafanyabiashara wakiwa ndio waratibu wakuu.

Katika hatua nyingine Loata Sanare amewaagiza Maafisa Biashara kutenda haki katika ugawaji wa vitambulisho hivyo huku akiwataka viongozi wengine wa Serikali kutorudia changamoto zilizojitokeza mwaka 2019.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuzindua zoezi hilo la kugawa vitambulisho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo alibainisha faida ya vitambulisho hivyo kuwa vinawawezesha wafanya biashara na watoa huduma wadogo wa sekta isiyo rasmi kufanya biashara zao bila kubughudhiwa.

Hata hivyo alibainisha changamoto zilizojitokeza mwaka jana kuwa ni pamoja na kutohifadhi kumbukumbu sahihi ya orodha ya majina ya wafanyabiashara na watoahuduma hao.

Changamoto ya pili ni wahusika wa kugawa vitambulisho hivyo kukaa na fedha mikononi mwao badala ya kupeleka Benki hivyo kuchelewesha uwasilishaji wa fedha hizo kwa wakati kwenye mamlaka husika  huku utoaji wa Elimu juu ya faida ya vitambulisho haukufanyika ipasavyo ikiwa ni changamoto iliyofanya vitambulisho hivyo kutochukuliwa kwa wingi.

Mkoa wa Morogoro kwa mwaka huu 2020, utapewa jumla ya vitambulisho 60,000 kwa mwaka mzima. Mkoa umekwishapokea jumla ya vitambulisho 12,000 ikiwa ni awamu ya kwanza na awamu ya pili Mkoa utaletewa Vitambulisho 48,000.

Baada ya Mkuu wa Mkoa kuzindua rasmi zoezi hilo la ugawaji wa Vitambulisho aliwakabidhi Wakuu wa Wilaya zote saba na kutakiwa kuanza kuvigawa mara moja ambapo Wilaya ya Kilosa imepata vitambulisho 2000, Ulanga 750, Gairo 900, Malinyi 620, Morogoro 3930, Mvomro 2000, na Kilombero vitambulisho1800.

Vitambulisho hivyo vitagawanywa kwa wale wafanyabiashara waliokidhi vigezo ikiwa ni pamoja na wale wenye biashara zao ambazo mauzo yake hayazidi Shilingi milioni Nne kwa mwaka na sio wenye mitaji isiozidi shilingi milioni Nne kwa mwaka.

Sharti jingine wafanyabiashara watakaopata vitambulisho hivyo ni wale ambao hawajawahi sajiliwa na TRA na kuwa na TIN namba.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.