• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

TFRA YAHAMASISHA MFUMO WA UNUNUZI WA MBOLEA WA PAMOJA

Posted on: April 13th, 2018

TFRA  YAHAMASISHA MFUMO WA UNUNUZI WA MBOLEA WA PAMOJA.

Mawakala wa kusambaza pembejeo za kilimo Mkoani Morogoro wametakiwa kuwa wavumilivu katika kuutekeleza mfumo mpya wa ununuzi wa pembejeo za kilimo unaowataka mawakala hao kununu pembejo hizo kwa pamoja wakati soko la pembejeo duniani linapokuwa chini.

Hayo yameelezwa na Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji mali Mkoa wa Morogoro Bw. Ernest Mkongo wakati akifungua Semina ya mafunzo ya siku moja kwa mawakala wa kusambaza pembejeo na wataalamu wa kilimo semina iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Aprili 12  mwaka huu.

Bw. Mkongo amesema kila lenye mwanzo halikosi changamoto hivyo ni jukumu la mawakala hao kuwa wavumilivu wanapokutana na changamoto zozote katika mfumo huu mpya ambao lengo lake ni kutaka kunufaisha Mawakala, Serikali na Wananchi kwa ujumla.

“Mfumo huu ndugu zangu ni mfumo mpya na kama tunavyo jua kitu kipya kinapoanza kinakuwa na changamoto zake”. Alisema Bw. Mkongo.

Katika kikao hicho, mtaalam wa elimu ya jamii kutoka TFRA  Bi. Rose Mdezi alisema kuwa mfumo wa BPS (Back procurement system) ambao unahusu ununuzi wa pamoja wa mbolea una lengo la likiwa ni kuhakikisha mbolea inanunuliwa kwa pamoja wakati bei ya mbolea katika soko la dunia ni ndogo ili itakapofika nchini  mkulima aweze kuipata kwa bei ya chini.

 ‘’Lengo letu kubwa sisi kama TFRA ni kuhakikisha wakulima wanapata mbolea kwa bei wanayoweza kuimudu’’ alisema Bi. Rose.

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa mawakala wa  kusambaza mbolea Mkoa  wa Morogoro  Michael Mpembwa alisema mpango huu ulio letwa na TFRA unaenda kutatua changamoto za mbolea ambazo wasambazaji wanakutana nazo. Alisema, awali Serikali haikuwa karibu na  mawakala kutokana na kutoshughulikia changamotowalizo kuwa wakikabiliana nazo lakini kwa sasa kupitia huu utaratibu watakuwa na ukaribu zaidi.

Naye Veronika Komba  ambae pia ni wakala wa mbolea alisema changamoto kubwa wanazokutana nazo licha ya serikali kuja na mpango huo ambao unaweza kusaidia kusambaza mbolea  kwa ufanisi ni Serikali kutolipa madeni yao kwa wakati na hivyo kusimamisha biashara zao na suala la bei elekezi ya pembejeo ambayo imepangwa bila kuzingatia umbali au utofauti wa mahali pembejeo inakopelekwa.

Kwa upande wake Afisa kilimo wa Mkoa wa Morogoro  Dk. Rozaria Rwegasila alisema mafunzo haya ya TFRA yatasaidia pande zote mbili kwa upande wa serikali na mawakala kwa kuwa elimu iliyotolewa inaelekeza mawakala namna ya kutatua changamoto walizonazo. Kuhusu madeni yanayodaiwa na mawakala, Dk. Rwegasira amesema Serikali inaendelea na uhakiki wa madeni hayo na mara itakapokamilisha wale wenye madeni halali watalipwa fedha zao.



Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • RC SANARE: NENDENI MKAJIFUNZE MALINYI.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.