• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

TUHUMA ZA KUKIMBIA NA FEDHA

Posted on: October 29th, 2019


Na. Andrew Chimesela - Morogoro.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ameiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Kilombero na  Mkoa wa Morogoro kumtafuta na kumkamata mtumishi mmoja wa Halmashauri ya Ifakara Mji kwa tuhuma za kukimbia na fedha za makusanyo ya halmashuri hiyo zaidi ya shilingi million 146.

Loata Sanare ametoa agizo hilo Oktoba 28 mwaka huu wakati wa ziara yake ya kujitambulisha wilayani Kilombero Mkoani humo kutumia fursa hiyo kuongea na watumishi wa Halmashauri ya Mji Ifakara na Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.

Pamoja na kuomba ushirikiano wa kutosha kutoka kwa watumishi wote wa Wilaya ya Kilombero Mkuu huyo ameendelea kufuatilia utekelezaji wa Maagizo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kasim Majaliwa Majaliwa aliyoyatoa wakati wa Ziara yake aliyoifanya mwezi Septemba mwaka huu Mkoani Morogoro.

Pamoja na kuzitaka Halmashauri zote kutekeleza haraka maagizo yote aliyoyatoa Waziri Mkuu, Sanare ameagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo kumtafuta na kumkamata mtumishi wa halmashauri ya Ifakara Mji Kassimu Chakachaka  ambaye  anatuhumiwa kutoroka na fedha za Halmashauri hiyo zaidi ya shilingi milioni 146.

Katika hatua nyingine Ole Sanare ameibebesha lawama Kamati ya Fedha ya Madiwani wa Halmashauri hiyo kwa kushindwa kusimamia fedha za Halmashauri hiyo kwa kuwa fedha nyingi zimepotea mikononi mwa watumishi wachache zikiwemo zaidi ya shilingi milioni 210 na nyingine kutumika pasipo kufuata utaratibu wa Kiserikali katika matumizi yake na wao kushindwa kuchukua hatua stahiki.

Pia Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero na Ifakara Mji kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wote waliosimamishwa kazi kwa tuhuma za  ubadhilifu wa fedha za serikali.

Naye Mtendaji Mkuu wa shughuli za Serikali Mkoa wa Morogoro ambaye ni Katibu Tawala wa  Mkoa huo   Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewataka watumishi wote wa Halmashauri ya Kilombero na Ifakara Mji pamoja na Mkoa mzima kuzingatia maadili katika utendaji wao wa kazi, Uzalendo na kutimiza majukumu yao kwa wakati.


Loata Ole sanare kwa kutembelea halmashauri hizo sasa atakuwa amebakiza Halmashauri mbili za Ulanga na Malinyi kukamilisha ziara yake ya kujitambulisha kwa halmashauri zote tisa katika Mkoa huo huku akipitia baadhi ya miradi kuona utekelezaji wake.


MWIISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.