• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Tusome Pamoja inavyoinua Kiwango cha Elimu Morogoro

Posted on: May 29th, 2019

“Tusome pamoja” inavyoinua kiwango cha Elimu Morogoro

Na. ndrew Chimesela - Morogoro

Imeelezwa kuwa mradi wa TUSOME PAMOJA unaotekelezwa Mkoani Morogoro umekuwa ni chachu katika kuinua kiwango cha Elimu Mkoani humo hususan katika shule za Msingi baada ya mradi huo kutumia dhana shirikishi katika utekelezaji wake.

Mafanikio hayo yameelezwa Mei 28 mwaka huu na Mwezeshaji wa Ushiriki Jamii wa Programu hiyo ya Tusome Pamoja Mkoa wa Morogoro Bw. Raphael Kibindo wakati wa ziara ya  ufuatiliaji wa utekelezaji wa Programu hiyo katika Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Mwezeshaji Raphael amesema sio kwamba Tusome Pamoja umemaliza kutatua changamoto za Sekta ya Elimu Mkoani humo lakini amesema mradi umeondoa kwa kiasi fulani tabia ya baadhi ya watendaji wa Serikali Katika Sekta ya Elimu ya kufanya kazi kwa mazoea hususan walimu  katika shule za Msingi na kwa sasa walimu  wanatumia mbinu zilizoelekezwa na Mradi katika kuwafanya wanafunzi waelewe “K” tatu yaani Kusoma, Kuandika na Kuhesabu.

“kwenye kila eneo imekuwa ikifanya kazi vizuri, utaona walimu wana stadi nzuri za kufundisha za kumfanya mtoto aweze kujifunza vizuri kusoma, kuandika na kuhesabu” alisema Bw. Raphael.

Aidha, Mwezeshaji Raphael ametoa Wito kwa Serikali hususan kwa Watendaji ngazi ya Wilaya na Kata kufanya ufuatiliaji katika kutekeleza azma ya Mradi huo kwa kufanya vikao vya mara kwa mara ili kujikumbusha majukumu yao na kutatua changamoto zinazojitokeza,  lengo ni mwanafunzi aelewe K tatu huku akiwataka Wazazi kwa kila shule kuona kuwa shule wanazosoma watoto wao ni mali yao.

Naye Afisa Elimu Mkoa wa Morogoro Mhandisi Joyce Baravuga katika ziara hiyo baada ya ufuatiliaji huo na kufanya mahojiano na Walimu Wakuu wa shule za Msingi na Waratibu Elimu wa Kata za Magomeni na Mkwatani Wilayani humo pamoja na changamoto zilizopo amekiri kuwa mradi huo ni chachu katika Elimu Wilayani Kilosa.

Hata hivyo,  Mhandisi Baravuga amehoji sababu ya zaidi ya shule 31 za Wilaya hiyo kutoingiza takwimu za shule zao kupitia Vishikwambi (Tablets) ambazo zimetolewa na Mradi wa tusome pamoja na kuziwasilisha ngazi za juu kwa kutumia Vishikwambi hivyo na kusababisha Wilaya ya kilosa kuwa nyuma katika utekelezaji wa Programu ya Tusome Pamoja.

Kwa sbabu hiyo, Mhandisi Baravuga ametoa mwezi mmoja kwa Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Kilosa Mwl. Christina Hauli kuwasimamia Waratibu Elimu Kata kuhakikisha kuwa ifikapo Juni 30 mwaka huu shule zote 158 za Wilaya ya Kilosa ziwe zimeingiza takwimu husika kupitia vishikwambi vyao vinginevyo hatua za kinidhamu zichukuliwa dhidi yao.

Mwezeshaji wa Ushiriki Jamii wa Programu ya Tusome Pamoja Mkoa wa Morogoro Bw. Raphael Kibindo (kulia)akitoa akitoa maelekezo kwa wajumbe wa kikao wakati wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa program hiyo Wilayani Kilosa.

Kwa upande wao Waratibu Elimu Kata na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi akiwemo Mwl. Mkuu Erick Yusuph wa shule ya Msingi Lamulilo Kata ya Magomeni Wilayani humo pamoja na kupokea maagizo ya Afisa Elimu Mkoa wanakiri kuwa Programu ya TUSOME PAMOJA  imewaleta pamoja baina yao na wadau wengine wa Elimu wakiwemo Umoja wa Wazazi – UWAWA.

Mwl. Yusuph ametaja maeneo ambayo UWAWA wameonesha ushirikiano kwa vitendo kuwa ni pamoja na suala zima la utoaji wa chakula kwa wanafunzi wa darasa la Saba na darasa la awali hali iliyoongeza mahudhurio shuleni na kupunguza idadi ya wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu katika shule zao.

Mradi wa TUSOME PAMOJA hapa nchini umeanza tangu mwaka 2016 na unatekelezwa Mikoa yote ya Zanzibar na Mikoa minne (4) ya Tanzania bara ambayo ni Iringa, Ruvuma Mtwara na Morogoro ukiwa na lengo la kuongeza na kuinua stadi za ufundishaji wa KKK kwa wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili ili wajue vema kusoma, kuandika na kuhesabu.

Mradi huu unatekelezwa kwa ufadhiri kutoka Marekani  (US AID)  na unatarajiwa kuisha mwaka 2021.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.