• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wataalam wa mifugo watakiwa kufanyia kazi mafunzo ya vikaokazi

Posted on: October 23rd, 2020


Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewataka Wataalamu wa Mifugo kufanyia kazi Elimu na ujuzi wanaoupata katika Mafunzo mbalimbali kwenye vikaokazi ili kuwasaidia wafugaji kufuga kisasa na kuboresha uchumi wao.

Mhandisi Kalobelo ametoa wito huo katika Kikao cha Mafunzo kwa Wakaguzi wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula na Mifugo kilichofanyika Oktoba 22 mwaka huu katika Ukumbi wa Engineering Bioprocessing uliopo SUA Mkoani Morogoro.

amesema wizara ya Mifugo na Uvuvi imeandaa mafunzo hayo kwa wataalamu hao kwa lengo maalumu ili watakaporejea katika maeneo yao waweze kuwasaidia wafugaji kutambua kuwa kufuga ni Uchumi.

Amebainisha mbele ya wajumbe wa kikao hicho kuwa imekuwa ni kawaida kwa watumishi waliowengi wanaoshiriki mafunzo kutoonesha elimu au ujuzi wanaopata kwenye mafunzo kwenye vikao kazi, hivyo kunakuwa hakuna tofauti kati ya mtumishi aliyepata mafunzo na ambaye hakupata mafunzo, badala yake anaendelea na utaratibu wake wa kila siku (business as ussually).


Sambamba na agizo hilo Kalobelo amewataka Wakaguzi hao mara tu baada ya kumaliza Mafunzo kuandika ripoti ya mafunzo hayo na kuonesha namna watakavyotoa Elimu hiyo kwa wafugaji katika  kuwezesha wazalishaji na wafugaji wa Vyakula vya Mifugo  kuendelea kufuga kisasa zaidi.

Aidha, Kalobelo amewataka Wakaguzi kufanya kazi zao kwa kusimamia Sheria, Kanuni  na Taratibu ili kulinda afya ya Walaji na Mifugo ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya kutosha kwa wadau waliopo kwenye mnyororo wa thamani kwenye Tasnia ya vyakula vya mifugo, kufanya hivyo kutatatua changamoto ya matumizi ya Vyakula na rasilimali za vyakula vya mifugo visivyo na ubora hapa nchini.

 “Mafunzo haya yawe chachu kwenu na kwa kuwasaidia wafugaji kuzalisha mifugo kwa tija kwa kutumia vyakula kutoka maeneo yaliyosajiliwa na kutambulika kisheria hatimaye kuongeza mchango wa Sekta ya Mifugo katika kuinua uchumi ngazi ya kaya na pato la nchi kwa ujumla”

Mafunzo ya Wakaguzi wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo yanatolewa ili kuwezesha kutatua changamoto za ubora na viwango hafifu vya vyakula vya mifugo vinavyotumiwa na wafugaji wengi kwani kumeonesha zipo athari za ukuaji hafifu kweye kuku,mbwa ,nguruwe na sungura.

Kikao hicho kilishirikisha wakaguzi wa maeneo ya malisho na Rasilimali za vyakula vya mifugo kutoka maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na wataalamu kutoka ngazi ya Mkoa, Wilaya na Serikali za Mitaa.

 

MWISHO.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.