• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Watoto milioni 8,082, 838 kupatiwa chanjo ya Surua na Rubella

Posted on: October 17th, 2019


Na Andrew Chimesela - Morogoro.

Watoto wapatao milioni 8,082, 838 wenye umri chini ya miezi tisa hadi umri wa miaka mitano Wanatarajia kupata chanjo ya Surua na Rbella  na wengine milioni 4, 041, 934 wenye umri wa mwaka mmoja na nusu watapatiwa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kupooza (Polio).

Hayo yamesemwa Oktoba 17 mwaka huu na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati akizindua Kampeni ya chanjo ya Surua, Rubella na Polio kwa mwaka 2019 iliyofanya kitaifa Mkoani hapa.

                                                                   RC Morogoro akimkaribisha rasmi mgeni wake katikauwanja wa Jamhuri kwa ajili ya kuzindua kampeni ya chanjo.

Aidha, Waziri Ummy Mwalimu amesema, hivi sasa Serikali kupitia Wizara hiyo inatoa chanjo tisa (9) ikiwa ni kinga dhidi ya magomjwa 13 yakiwemo magonjwa ya kifua kikuu, Kupooza, Kifaduro, donda Koo, Pepopunda, homa ya ini, Kichomi, Uti wa mgongo, Mafua makali, kuhara, Surua, Rubella na Saratani ya mlango wa kizazi.

“Ni dhahiri kuwa haya ni mafanikio makubwa ikilinganishwa na mwaka 1975 tulipokuwa tukitoa chanjo dhidi ya magonjwa  ya matano tu” amesema Waziri Ummy.

Aidha, amesema zoezi la Kampeni hiyo litagharimu takribani Tsh. Bilioni 11.9 sawa na dola za kimarekani Milioni 4.59  huku lengo kuu likiwa ni kushiriki katika mkakati wa kimatifa katika kutokomeza ugonjwa wa surua na Rubella ili kuchangia katika kupunguza vifo vya watoto hapa nchini.

                                                                              Waziri wa afya Ummy Mwalimu akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo.

Waziri Ummy amesema tayari Tanzania imefanikiwa kufikia lengo la Milenia la kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka mitano kutoka vifo 104 kati ya vizazi hai1000 kwa mwaka 2004/2005 hadi vifo 54 kati ya vizazi hai 1000 mwaka 2013.

Naye mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk. Ketsela Mengistu amesema Shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutokomeza magonjwa yanayozuilika kwa chanjo.

Dkt. Ketsela amewataka watanzania kushiriki kikamilifu katika Kampeni hizo ili kusaidia kupunguza vifo vya watoto vinavyotokana na magonjwa hayo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Loata Ole Sanare amesema, Jumla ya watoto 328, 462 wanatarajiwa kupata chanjo ya Surua na Rubella huku watoto 136,764 watapatiwa chanjo ya Polio Mkoani humo.

Amesema, Kampeni hizo hufanyika kila baada ya miaka mitatu ambapo mara ya mwisho ilifanyika mwaka 2014 wakati chanjo ya Rubella ilipoanza kutolewa kwa mara ya kwanza ambapo ilianza kwa watoto wa chini ya miaka 15.

Kampeni hii inatarajiwa kufanyika kitaifa kwa siku tano (5) kuanzia Oktoba 17 hadi Oktoba 21 itakapohitimishwa huku kauli mbiu ya Kampeni hiyo ikiwa ni “Chanjo ni Kinga , kwa pamoja tuwakinge”

mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.