• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Watumishi RS Morogoro wamwagiwa sifa, watakiwa kushiriki kupiga kura

Posted on: October 23rd, 2020

Watumishi RS Morogoro mwagiwa sifa, washauriwa kushiriki kupiga kura.

Na, Andrew Chimesela, Morogoro

Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wamepongezwa na Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo kwa kufanya kazi kwa bidii hivyo kuwaondolea wananchi kero mbalimba walizozifikisha ofisini hapo.

Mhandisi Kalobelo ametoa pongezi hizo kwa watumishi hao Oktoba 23 mwaka huu katika kikao kilichoshirikisha Wakuu wa Idara na Vitengo katika Ofisi hiyo ili kuwakumbusha kutekeleza majukumu yao lakini pia kutathmini utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Akizungumzia suala la kufanya kazi kwa bidii, Mhandisi Kalobelo amesema Watumishi katika Ofisi hiyo wametembea na kauli mbiu ya Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya “HAPA KAZI TU” kwa kuwa wamejituma kufanya kazi kwa bidii hususan katika kuwaondolea adha wananchi wa Mkoa huo kupitia ushauri wa kitaalamu walioutoa.

“kingine ambacho kimenipa faraja kufanya kazi na ninyi, ni pale tunapowataka mtoe maelezo Fulani au utaalamu Fulani kwa kweli mnajitahidi kutoa ushauri wa kitaalamu” alisisitiza Mhandisi Kalobelo.


Katika hatua nyingine Katibu Tawala huyo wa Mkoa ambaye ndiye mwajiri wa watumishi hao ametoa wito kwa watumishi wote kushiriki kikamilifu kwenye zoezi muhimu la Uchaguzi Mkuu katika kuchagua viongozi kwa nafasi ya Urais, Ubunge na Madiwani, ambalo linatarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.

Akimwakilisha Katibu Tawala Msaidizi Utumishi na Utawala, Victor Ndiva ambaye ni Afisa Tawala amesema ingawa kikao hicho ni cha kawaida ambacho hufanyika ili kuwakumbusha watumishi kutekeleza wajibu wao, kikao kimejikita katika kutathmini namna nzuri ya utoaji huduma kwa wananchi ili kuenenda na lengo la Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli ya kumsaidia mwananchi hususan wa hali ya chini.


Kwa upande wake Annamary Mwasendwa mmoja wa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa amewakumbusha wananchi kufika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupata huduma wanazohitaji bila kutumia ushawishi wowote katika kupata huduma hiyo ikiwa ni pamoja na kutomshawishi mtoa huduma hiyo kumpa zawadi, kwani kufanya hivyo ni sawa na kutoa rushwa.

Naye ni Enock Juriely ambaye ni Afisa Elimu anayeshughulikia Elimu kwa TEHAMA, ameishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kuratibu vema kikao hicho ambacho ndani yake wamejifunza mbinu mpya za utoaji huduma kwa wananchi hivyo kuendelea kutoa huduma hiyo kwa ubora zaidi.


MWISHO

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.