• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Watumishi wa RS wapewa Somo

Posted on: August 12th, 2020

Watumishi RS Morogoro wakumbushwa kujiandaa kimaisha.

Na Andrew Chimesela – Morogoro

Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro wamekumbushwa na kuhimizwa kujiandaa kimaisha kwa kupanga mipango yao vizuri kuanzia sasa badala ya kutegemea kupanga mipango hiyo baada ya kustaafu.

Rai hiyo imetolewa Agosti 12 mwaka huu na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo alipozungumza nao muda mfupi baada ya Maafisa wa Benki ya NMB kufika na kutoa mada kuhusu huduma zinazotolewa na Benki hiyo na kuwahamasisha watumishi hao kwenda kuchukua mikopo iliyo na riba nafuu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo akiongea na Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa (Hawapo pichani)

Mhandisi Kalobelo amesema Mtumishi wa Serikali akiwa na uhakika wa maisha ya baadae ni dhahiri anaweza kufanya kazi vizuri katika utumishi na hata kuishi maisha marefu baada ya utumishi wake kuliko kama atakuwa hana uhakika wa maisha kutokana na kutojiandaa mapema kimaisha.

“tujitahidi kwa kadri tunavyoweza tuwe na mipango mizuri ya kuitumia mishahara yetu kwa kupata mikopo kwenye instituions (Taasisi) zilizopo” Amesema Mhandisi Kalobeli

Meneja wa Wateja Benki ya NMB Tawi la Wami Masanja Manyilizu akitoa mada kwa Watumishi wa RS Morogoro.

Aidha, amewatahadharisha watumishi hao kuchukua mikopo na kuanzisha miradi waliyoipanga wenyewe badala kuanzisha miradi kwa kufuata mikumbo ya watu na zaidi ametaka kupata ushauri wa kuanzisha miradi yao kutoka kwa Taasisi walizokopa fedha mikopo hiyo.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo ambaye ni mtendaji Mkuu wa Serikali ngazi ya Mkoa amesema nchi yetu ina Amani kwa muda mrefu ambayo inatokana na familia nyingi kuwa na amani, kwa msingi huo ametaka watumishi hao hususan ambao wako kwenye maisha ya ndoa kuishi maisha ya uaminifu ili Amani iweze kuimarika ndani ya familia na kudumisha msemo wa Tanzania ni kisiwa cha Amani.

Picha mbalimbali hapo juu ni Watumishi wa RS wakiwa katika Kikao hicho

Kwa upande wake Meneja wa Wateja kutoka Benki ya NMB tawi la Wami Mkoani hapa Bw. Masanja Manyilizu pamoja na kusisitiza kuwa Benki hiyo ina usalama wa uhakika katika kutunza pesa za wateja wao, amewataka watumishi hao kutokuwa na Imani yoyote katika masuala ya fedha hususan kutoa namba za siri za akaunti za benki kwani kufanya hivyo ni kuhatarisha usalama wa fedha zao.

Aidha, Manyilizu amewataka watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa kufika katika Benki yao na kupata mikopo ya aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na mikopo ya nyumba yenye riba ndogo badala ili kjiandaa mapema kimaisha kuliko kutegemea mishahara kwani mishahara yao ni daraja la wao kuwa na maisha bora.


Afisa Tawala Idara ya Utumishi na Utawala akiteta jambo na Afisa wa Benki ya NMB Tawi la Wami mara baada ya kikao hicho (picha zote na Andrew Chimesela)

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE ATATUA MGOGORO WA ARDHI.

    April 13, 2021
  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.