• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Kakunda Atoa Wito Kwa Watanzania

Posted on: February 17th, 2019

Waziri Kakunda atoa wito 

Waziri wa Viwanda na Biashara Joseph Kakunda amewataka watanzania kuondokana na dhana potofu iliyojengeka miongoni mwao ya kudharau bidhaa zinazotengenezwa katika viwanda vya hapa nchini badala yake ametoa wito kuzipende bidhaa hizo kwani zina sifa na ubora unaohitajika.

Waziri Kakunda ametoa wito huo Februari 16 mwaka huu wakati wa ziara yake ya siku moja Mkoani Morogoro alipotemmbelea Kiwanda cha kutengeneza Magunia na kiwanda cha kutengeneza nguo cha Twenty First Century  ambavyo vyote viko Kihonda katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Baada ya kutembelea kiwanda hicho na kujionea mwenyewe nguo zinazotengenezwa kiwandani hapo huku zikiwa na ubora wa kimataifa, akatoa wito kwa Watanzania kutodharau bidhaa zinazotengenezwa hapa nchini badala yake kuzithamini na kuzipenda.

 “watanzania hawapendi vitu ambavyo vimetengenezwa made in Tanzania wanadharau… Natoa wito kwa watanzania waanze kupenda vitu ambavyo vinavyotengenezwa Tanzania” alisema Waziri Kakunda.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe alimueleza Waziri Kakunda kuwa kiwanda cha Twenty First Century  ambacho awali kilijulikana kama Morogoro Polyester  ni moja ya viwanda 16 ambavyo vilijengwa na hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambacho pamoja na kiwanda cha Mazava kinachotengeneza nguo za michezo vinatoa ajira kwa watanzania zaidi ya 5,000.

Aidha, Waziri Kakunda alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro pamoja na viongozi wengeni wa Mkoa huo kwa kusimamia ufufuaji na ujenzi wa viwanda Mkoani humo na kuufanya Mkoa wa Morogoro kuanza kurejea kwenye hadhi yake ya zamani ya kuwa  Mkoa wa Viwanda.

Naye meneja Uzalishaji wa Kiwanda hicho cha Kutengeneza Nguo Bw. Clementi Munisi alisema kiwanda chao kina uwezo wa kutenngeneza nguo zenye viwango vyote Duniani na wanaweza kushindana na nchi yoyote Duniani katika soko la kutengeneza nguo.

Kabla ya kutembelea kiwanda cha nguo, Waziri Kakunda alitembelea kiwanda kinachotengeneza magunia ambapo aliagiza Uongozi wa Kiwanda kutofunga kiwanda hicho kwa kuwa Serikali imekwisha pokea changamoto za kiwanda  na inazifanyia kazi.

Akitoa taarifa ya kiwanda, Meneja wa Kiwanda hicho Ndekirwa Mnyari alimweleza Waziri kuwa kiwanda kina uwezo wa kuzalisha magunia milioni kumi kwa mwaka na kwa sasa kinatengeneza magunia yasiyozidi milioni mbili tu kwa mwaka, aidha kiwanda kwa sasa kina magunia laki tano ambayo yamekosa soko hali inayosababishwa na uingizwaji wa magunia kutoka nje ya nchi.

AFISA HABARI

OFISI YA MKUU WA MKOA

MOROGORO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.