• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Bajeti ya Serikali 2022/2023 yatekelezwa kwa 96%.

Posted on: September 8th, 2023

Watendaji wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wamepongezwa kwa utendaji mzuri katika utekelezaji wa shughuli za Serikali kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 ambayo imetekelezwa kwa asilimia 96.

Pongezi hizo zimetolewa Septemba 07 mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Natu El-Maamry Mwamba wakati akifunga kikao kazi cha siku tatu cha tathmini ya utekelezaji wa bajeti ya 2022/2023 na maandalizi ya bajeti ya 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa NSSF uliopo Manispaa ya Morogoro.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame akizungumza na washiriki wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema ushirikiano katika kutekeleza bajeti hiyo umewezesha kupata mafanikio katika utekelezaji wa shughuli za Serikali ambapo kwa asilimia 96 shughuli hizo zimefanikiwa hivyo amewashukuru na kuwapongeza kwa ushirikiano na utendaji kazi mzuri.

“...nitumie fursa hii kuwashukuru kwa ushirikiano na utendaji kazi mzuri katika utekelezaji mzuri wa bajeti ya 2022/2023 uliotuwezesha kupata mafanikio ambapo kwa asimilia 96 tumefanikiwa...” amesema Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame.

Aidha, amesema kuwa Serikali itayafanyia kazi maoni yaliyotolewa na washiriki wa kikao hicho kwa kuwa wao ndiyo watekelezaji wakubwa wa bajeti katika maeneo yao.

Sambamba na hilo Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame amesema Serikali imezipokea changamoto zilizoibuliwa na wajumbe wa kikao hicho hususan katika uandaaji wa bajeti na kuahidi kuzifanyia kazi ili kuboresha utekelezaji wa bajeti hiyo.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Mipango na Uratibu Bw. Anza-Ameni Ndosa amesema kikao hicho kimelenga kujadili changamoto mbalimbali za utekelezaji wa bajeti na namna ya kutatua changamoto hizo.

Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Mipango na Uratibu Bw. Anza-Ameni Ndosa akiwa kwenye kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Bajeti ya Serikali 2022/2023.

Naye, Bw. Edson Toto ambaye ni Mchumi kutoka Wizara ya Fedha amesema kikao hicho kimehusisha washiriki kutoka Mikoa 13 ambapo Maafisa Mipango wa Mikoa na Halmashauri, Maafisa Rasilimali watu na Wahasibu ni walengwa wa kikao.

Akitoa shukrani kwa niaba ya washiriki  wa kikao hicho Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Mipango na Uratibu wa Mkoa wa Njombe Bw. Edward Mwakipesile ameshukuru na kuahidi kuyafanyia kazi  maelekezo waliyoyapata kwenye mafunzo ili kupata mafanikio chanya katika utekelezaji wa shughuli za Serikali katika maeneo yao.

Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Mipango na Uratibu kutoka Mkoa wa Njombe Bw. Edward Mwakipesile akitoa neno la shukran kwa mgeni rasmi pamoja na kwa waandaaji wa kikao kazi hicho.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.