• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Daraja la Luipa laondoa kadhia kwa wakazi wa Mlimba.

Posted on: April 16th, 2025

Ujenzi wa miundombinu bora ya barabara na daraja la luipa imewasaidia  kwa kiasi kikubwa wananchi wa  vijiji vya misegese, Chiwachiwa na Lavena vilivyopo kata za Namawala na Mbingu Halmashauri ya Mlimba na kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa na mazao kwa urahisi.


Hayo yamebainishwa Aprili 16, 2025 na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ndugu Ismail Ali Ussi wakati akifungua daraja hilo katika kijiji cha misegese ambalo limegharimu zaidi ya Tsh. Bil. 1.9.


Aidha, Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge kitaifa amesema hapo mwanzo daraja la Luipa lilikuwa kikwazo kwa wananchi katika kusafiri na kusafirisha bidhaa mbalimbali kwa sasa kero hiyo imekwisha baada ya daraja hilo kujengwa na kukamilika chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suhulu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


"...daraja hili lilikuwa changamoto kwa wananchi wetu kutoka eneo moja kwenda jingine lakini kwa mapenzi aliyonayo Rais Samia leo hii tunajionea daraja la kisasa na shughuli zetu za maendeleo tunaweza kufanya muda wowote..." amesema Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge


Sambamba na hayo ndugu Ismail amewataka wananchi kutunza na kuthamini miradi ya maendeleo ambayo serikali inayotumia fedha nyingi kuibuni na kujenga ili kukuza uchumi wa jamii na nchi kwa ujumla hivyo jamii inapaswa kuitunza na kuendelea kutumika vizazi na vizazi.


Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mlimba Mhe. Godwin Kunambi amesema mbali na daraja hilo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suhulu Hassan ameazimia kujenga madaraja mengine sita ya kiwango cha juu katika vijiji vya Chiwachiwa, Isago, Mpanga, Mfuji na Mbasa ili kuboresha miundombinu ambayo ndio chachu ya maendeleo.


Awali akitoa taarifa ya daraja hilo, Mhandisi Nurdin Msengi kwa niaba ya Meneja wa Wakala wa barabara za mjini na vijijini (TARURA) Wilaya ya Kilombero amesema mradi huo umerahisisha wananchi kufika maeneo ya huduma za Kijamii na Kiuchumi kwa wakati hususani wakati wa masika na kutumika kama barabara ya kimkakati ya kukuza uchumi wa Halmashauri ya Mlimba Wilayani kilombero ili kuwa kitovu cha mapato kwa manufaa ya Taifa.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.