• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DC SHAKA ASISITIZA MALEZI BORA KWA WATOTO.

Posted on: March 31st, 2025



Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Mhe. Shaka Hamdu Shaka, amewasisitiza walezi wa vituo vya kulelea watoto wenye mahitaji maalum Mkoani Morogoro kuwalea watoto hao kwa misingi yenye maadili mema na yanayompendeza Mungu, ili kuwa na kizazi bora cha baadae.

Mhe. Shaka amesema hayo wakati akikabidhi zawadi za Eid Al-Fitr, kwa watoto wa vituo vinne vya kulelea watoto wenye mahitaji maalum vya Mkoani Morogoro akimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima, zawadi ambazo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na kusisitiza kuwa maadili ndiyo nguzo kuu ya kudumisha amani na utulivu hapa nchini.

Mkuu huyo wa wilaya amesema, ni jukumu la walimu na walezi kuwalea watoto hao katika maadili mema, huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya mazingira yao hususan ya shule na vituo vya malezi, ili watoto hao wapate elimu itakayowawezesha kujitegemea kiuchumi kwa siku za usoni.

"Endeleeni kuwalea watoto hawa kwa misingi inayompendeza Mwenyezi Mungu ili tuwe na kizazi bora cha baadaye," amesisitiza Mhe. Shaka.

Aidha, Mhe. Shaka ameihimiza jamii kutambua kuwa jukumu la kuwalea watoto yatima, wenye mahitaji maalum na wanaotoka katika mazingira hatarishi si jukumu la walezi wa vituo hivyo pekee au la serikali, bali ni la jamii nzima.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa wa Morogoro, Bi. Amisa Amir Kagambo, amesema jumla ya vituo vinne vya makao ya waoto wenye mahitaji maalum na cha kituo kimoja cha kurekebisha tabia (Geleza la wafungwa Kilosa) vimetembelewa huku akiweka bayana kuwa zaidi ya watoto 300 wameguswa na mkono wa Eid na kutumia fursa hiyo kumshukuru Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa kusimamia zoezi hilo hadi kufanikiwa.

Naye Shekhe wa Wilaya ya Kilosa, Bw. Nasoro Mirambo, alimshukuru Rais Samia kwa kuwakumbuka watoto hao wenye uhitaji, akisema kuwa kitendo hicho ni faraja kubwa kwao, kwa wazazi wao, ndugu na hata kwa jamii nzima.

Baadhi ya watoto waliopokea zawadi hizo waliiomba jamii iendelee kuwakumbuka na kuwasaidia. Miongoni mwa watoto waliotoa shukrani na maombi hayo ni pamoja na Brayton Adi, alimshukuru Mhe. Rais kwa zawadi alizowapati akisema, "Mhe. Rais siyo tu kiongozi wa nchi, bali pia ni mlezi wao.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.