• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA BUNGE YA TAMISEMI KUKAGUA MIRADI YA SEQUIP, BOOST MOROGORO.

Posted on: February 19th, 2024

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI inatarajia kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo ya Sekta ya Elimu Mkoani Morogoro inayotekelezwa chini ya mradi wa kuimarisha elimu ya Sekondari – SEQUIP na kuimarisha elimu ya Awali na Msingi – BOOST katika Halmashauri Nne za Mkoa huo.

Hayo yamebainishwa Februari 19, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati akitoa taarifa ya miradi hiyo ambayo moja ya miradi itakayotembelewa ni Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Morogoro iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro DC.

Akitoa taarifa ya miradi hiyo Mkuu wa Mkoa huo amegusia changamoto ya Mradi wa Sekondari ya Wasichana ya Morogoro huku akiiomba Kamati hiyo ya Bunge kutupia jicho la pekee mradi huo kutokana na changamoto kubwa iliyopo katika utekelezaji wake mradi ambao unagharimu jumla shilingi Bil. 3.

“...hili la shule ya sekondari ya bilioni tatu…kuna kamati ya usimamizi lakini ule muundo mzima wa kusimamia ile hela ni jambo la ajabu sijawahi kuona…” amesema Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dennis Londo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mikumi kwa niaba ya wajumbe wengine wa Kamati hiyo ameonesha dhamira yao ya kuitaka Serikali kudhibiti matumizi mabaya ya fedha zinazotokana na mapato ya Halmashauri kwa kuwa amesema fedha zinazotoka Serikali Kuu zinalemaza Halmashauri nyingi hapa nchini.

Aidha, Mwenyekiti huyo ameeleza kwa ufupi maazimio ya kamati hiyo ambayo yatajadiliwa kipindi cha Bajeti kuwa ni pamoja na masuala mtambuka kama suala la Lishe, taulo za kike, ukusanyaji na matumizi na mapato ya ndani, viwanja vya michezo na miundombinu ya shule kama vile vyoo, Madarasa na utoshelevu wa madawati.

Katika hatua nyingine, Mhe. Dennis Londo amempongeza Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima kwa ubunifu wake kwa kuzifanyia tathmini Halmashauri za Mkoa huo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wao na kuimarisha usimamizi wa fedha za Serikali wanazokusanya katika Halmashauri zao na zile zinazopokelewa kutoka Serikali Kuu.

Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa, Kamati hiyo itatembelea Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Mvomero, Kilosa, Ifakara na Halmashauri ya Mlimba kuanzia Februari 19 hadi Februari 24, 2024.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.