• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Katibu Mkuu TAMISEMI atoa maagizo kwa Maafisa Nchini.

Posted on: January 4th, 2024

Katibu Mkuu TAMISEMI atoa maagizo kwa Maafisa Elimu Nchini.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Adolf Ndunguru amewaagiza Maafisa elimu wote wa Mikoa na Halmashauri hapa Nchini kukamilisha ujenzi wa miradi ya Elimu inayotekelezwa katika maeneo yao kabla au ifikapo Januari 15, mwaka huu.

Katibu Mkuu huyo ametoa maqgizo hayo Januari 4, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha Makatibu Tawala wasaidizi Idara ya Elimu pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Glonency iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Kikao kazi hicho kilichokuwa na kauli mbiu isemayo, uwajibikaji wenye ubora ubunifu na uadilifu ni msingi muhimu katika kuboresha elimu msingi na sekondari Nchini kinalenga kuweka mikakati ya pamoja kwa ajili ya mwaka 2024, ili kuweza kusimamia masuala ya elimu na kupata mafanikio.

Aidha, Aldof Ndunguru amewataka Maafisa hao kusimamia kikamilifu ufundishaji na ujifunzaji mashuleni na kuhakikisha walimu wasiotimiza wajibu wao kuchukuliwa hatua stahiki, pia kuhakikisha wanafunzi wote wa darasa la tatu na kidato cha kwanza wanamudu stadi ya lugha ya kingereza ifikapo mwishoni mwa mwaka.


“….. Hakikisheni miradi yote inayotekelezwa kwenye maeneo yenu ya usimamizi inakamilika kabla au ifikapo januari, 15 2024...” amesema Adolf Ndunguru.

Pia Ndungulu amesema chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan tunashuhudia uwezeshaji mkubwa wa rasilimali fedha katika sekta ya Elimu hapa Nchini kwa kugharamia elimu msingi bila ada ya shilingi bilioni 33.3 kila mwezi na kupanua wigo wake hadi kufika kidato cha sita.


Amesema katika kipindi cha mwaka 2020-2021 hadi 2023-2024 serikali imetoa trilioni 1.41 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule za awali msingi na sekondari, ambapo fedha hizo zimejenga shule mpya 380 vyumba vya madarasa 8964, mabweni 46, matundu ya choo 25688, nyumba za walimu 857, ujenzi wa mabwalo 6 na ukarabati wa shule za vituo vya walimu 396 wa elimu ya awali na msingi.

Katika hatua nyingine akibainisha kwa upande wa rasilimali watu amesema jumla ya walimu 28179 wameajiriwa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2020-2021 na 2022-2023 wakiwemo walimu 16542 wa shule za awali na msingi na walimu 11637 wa shule za sekondari.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu Charles Msonde amewapongeza walimu kwa kusimamia vizuri elimu ya awali na msingi hivyo kupelekea wanafunzi wa darasa la kwanza kuweza kusoma, kuandika na kuhesabu.

Amebainisha kuwa hadi kufikia septemba 30 mwaka jana ongezeko lilifikia asilimia 97% ya wanafunzi wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu pia kwa darasa la tatu kutoka asilimia 35% hadi kufikia asilimia 75% kwa wanafunzi wanaojua kuongea lugha ya kingereza.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.