• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

LISHE BORA NI HAKI YA KILA MTOTO, SOTE TUWAJIBIKE

Posted on: August 8th, 2022

Lishe bora na huduma zingine za msingi kama elimu na afya ni haki ya kila mtoto kwa mujibu wa Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  lakini mara nyingi watoto hukosa  lishe bora kutokana na sababu mbalimbali, zikiwemo hali ya kipato, kutokuwa na elimu sahihi kuhusu Lishe bora pamoja na mila na desturi za jamii.


Amesema hayo agosti 8, 2022 katika kikao cha kufanya tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.


"udumavu huu wa akili hupelekea mamilioni ya watoto kuwa na tatizo la akili na kusababisha tatizo kwa jamii nzima... tunatakiwa kutoa elimu ya Lishe bora, kwani ni haki ya Msingi kwa kila mtoto kwa maendeleo ya jamii..." amesema Mhe. Fatma Mwassa


Mhe. Mwassa amesema hali hiyo  inaweka afya za watoto hatarini kwani hupelekea tatizo la udumavu wa akili na kujenga jamii yenye tatizo la Afya ya akili, na utapiamlo kwa kukosa lishe bora, lakini wengine hata hushindwa kuhudhuria masomo katika shule zao.


Nae Bi. Salome Magembe, Afisa Lishe Mkoa wa Morogoro amesema  kuna idadi kubwa ya watoto wenye udumavu ambapo utafiti uliofanyika mwaka 2018 ulionesha 26.4% sawa na watoto 100,730 wana udumavu kwani hali hiyo hupunguza nguvu kazi kimwili na kiakili na kuchochea changamoto za uzalishaji katika Taifa. 


Sambamba na hilo, Bi. Salome amesema mikakati iliyowekwa katika kikao hicho ni kutoa elimu ya lishe kwa jamii kupitia viongozi mbalimbali wakiwemo maafisa watendaji wa Kata na maafisa Lishe waliopo katika Halmashauri zote 9 za Mkoa wa Morogoro.


Kwa upande wake, Bw. Simon Mkali Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mlimba, Mkoani Morogoro amesema mila na desturi ni changamoto kubwa kwa jamii hizo kwani wazazi hushindwa kuwanyonyesha watoto wao ipasavyo, sambamba na hilo amesema kuwa wanajukumu kubwa la kuelimisha jamii ili kujenga jamii yenye uelewa kuhusu Lishe bora.


Mwisho.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.