• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mashirika yasiyo ya Kiserikali yatakiwa kupanua wigo wa huduma kwenye maeneo yenye uhitaji.

Posted on: September 8th, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame akizungumza na wadau wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoani Morogoro wakati akifungua mkutano wa mwaka wa Mashirika hayo.

Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoani Morogoro yametakiwa kupanua wigo wa utoaji huduma kwenye jamii katika maeneo ambayo hayajafikiwa ili kutoa fursa ya sawa kwa huduma zinazotolewa.

Hayo yamesemwa Septemba 07 mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Bw. Jabir Makame kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima  wakati akifungua mkutano wa mwaka wa mashirika hayo yaliyopo Mkoani Morogoro uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Bw. Makame amesema baadhi ya mashirika hayo hutekeleza shughuli zake kwa kuchagua maeneo hususan maeneo ya mijini hivyo kupunguza fursa kwa maeneo mengine kupata huduma zinazotolewa na mashirika hayo, hivyo ameyataka mashirika hayo kuyafikia maeneo ambayo yanauhitaji hususan maeneo yaliyo pembezoni mwa mji.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame akibadilishana mawazo na mtaalam wa elimu kwa mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakati wa mkutano wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali.

“...naomba nitoe msisitizo kwamba katika kutekeleza majukumu yenu ni vyema pia kuangalia maeneo ambayo yanauhitaji vile vile ikiwemo katika Wilaya zingine za pembezoni...utakuta mashirika mengi yapo mjini...” amesema Jabiri Makame.

Aidha, amesema kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inatambua mchango wa Mashirika hayo katika kuleta maendeleo kwenye sekta mbalimbali za Afya, elimu, maji, mazingira, kilimo, upingaji wa vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na uimarishaji wa uchumi wa kaya.

Sambamba na hilo, Mkuu huyo wa Wilaya ameyataka mashirika hayo kutojikita katika miradi ambayo ni kinyume na mila, tamaduni na maadili ya Watanzania na kwamba Serikali haitashindwa kuyachukulia hatua mashirika yatakayo jihusisha na ukiukaji wa tamaduni za watanzania.

Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Rasilimali watu na Utawala Bw. Herman Tesha akizungumza wakati wa mkutano wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoani Morogoro.

Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Mipango na Uratibu Bw. Anza-Ameni Ndosa akifafanua kuhusu umuhimu wa mkutano hyo.

Kwa upande wao wadau wa Mashirika hayo Mkoani humo akiwemo Mjumbe wa Uratibu kutoka Taasisi ya Acts of Life Dkt. Francis Nyakamwe amebainisha changamoto zinazoyakabili mashirika yasiyo ya kiserikali Mkoani humo zikiwemo ukosefu wa rasilimali fedha, sheria kandamizi zinazowabana katika utendaji kazi zao, wingi wa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambazo hawana uelewa nazo.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame akiwa kwenye picha za pamoja na makundi mbalimbali ya wadau wa Mashirika yasiyo Kiserikali baada ya ufunguzi wa mkutano hyo.

Aidha, wadau hao wamependekeza kuwepo kwa miongozo ya moja kwa moja ya usajili hii ni kutokana na changamoto ya mashirika hayo kutakiwa kusajiliwa kwa mara ya pili hususan kwenye maeneo wanayokwenda kutekeleza shughuli zao.

Kikao hicho kimelenga kujadili kwa pamoja namna ya kutatua changamoto zinazoyakabili mashirika hayo pamoja na Serikali kutoa maelekezo kwa mujibu wa sheria, kanuni na sera zinazotolewa mara kwa mara.

MWISHO.

Matangazo

  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro April 13, 2023
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • View All

Habari Mpya

  • Serikali yatatua mgogoro wa wananchi wa Mindu, 367 kulipwa kifuta jasho

    September 23, 2023
  • Serikali yatatua mgogoro wa wananchi wa Morogoro, 367 kulipwa kifuta jasho

    September 23, 2023
  • RC Malima aitaka TRA kutoa elimu kwa wazalishaji kuongeza ukusanyaji kodi

    September 22, 2023
  • RC Malima ataka TRA kutoa elimu kwa wazalishaji kuongeza ukusanyaji kodi

    September 22, 2023
  • View All

Video

Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.