• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mwili wa aliyekuwa mke wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro waagwa, Waziri Ummy aongoza shughuli ya kuuaga.

Posted on: January 22nd, 2022

Mwili wa aliyekuwa mke wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro waagwa, Waziri Ummy  aongoza shughuli ya kuuaga.

Mwili wa aliyekuwa mke wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bi. Magdalena Layda Shigela umeagwa leo Jan. 22, 2022 huku viongozi mbalimbali wa chama na Serikali pamoja na waombolezaji wakishiriki kuuga tayari kwa safarishwa  kwenda Kishapu Mkoani Shinyanga kwa maziko.

Shughuli ya kuaga mwili wa marehemu Magdalena imeongozwa na Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (Mbunge) nyumbani kwa marehemu Salasala, Mtaa wa Kilimahewa Jijini Dar es Salaam akishirikiana na viongozi wengine wa chama na Serikali akiwemo Waziri wa Madini Dotto Biteko na Katibu wa Chama cha Mapinduzi Taifa Daniel Chongolo pamoja na Naibu wake Cristine Mndeme.

Akiwasilisha salamu za Serikali, Waziri Mwalimu ametoa pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela kwa kuondokewa na Mpendwa wake na kwamba kwa niaba ya Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi wengine wa serikali anatoa pole na wako pamoja katika kipindi hiki kigumu.

“Naomba pia upokee salamu zao za pole kwa niaba yao, hatuna mengi ya kusema kwa sababu hayo ni matakwa ya mwenyezi Mungu” amesema Waziri Ummy.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Bi. Christine Mndeme pamoja na kuwataka waombolezaji kumuombea marehemu Magdalena, amewataka pia ndugu, jamaa, marafiki na waombolezaji waliofika kwenye msiba huo kuyaenzi yote mazuri aliyoyafanya Magdalena enzi za uhai wake.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Martine Shigela akiwa na watoto wake Lorenzo na Loveness wakati wa kuaga mwili wa mke wake Bi.Magdalena Layda Shigela.

Akitoa salamu za pole kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa wote Tanzania Bara, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Wilbert Ibuge amesema wakuu wa Mikoa wanatambua uzito alionao Martin Shigela pamoja na familia yote kwa kuondokewa na Mpendwa wao na kwamba kazi nyingi za Kiserikali alizofanikiwa kuzifanya shigela zinatokana na maisha ya Amani, utulivu na Upendo uliokuwa umetawala katika familia yao, hivyo anahitaji  kuombewa zaidi kustahimili kipindi kigumu anachopitia.

Wakiwasilisha salamu za Mkoa wa Morogoro, Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi Mkoa wa Morogoro Mhe. Dorothy John amemtaka Kiongozi wao Mhe. Martine Shigela kumtegemea mungu katika kipindi anachopitia, huku Katibu Tawala wa Mkoa huo Bi. Mariam Mtunguja kwa ya watumishi wote wa Serikali Mkoa wa Morogoro ametoa pole nyingi kwa Mhe. Martine Shigela na familia nzima na kuwatakia utulivu wa moyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro martine Shigela pamoja na kuwashukuru watu mbalimbali kwa namna ambavyo wamejaribu kuokoa maisha ya mkewe bila mafanikio na namna walivyomkimbilia wakati wa msiba amesema msiba huo kwake ni mzito na unapelekea kuanza upya maisha mengine kwa uzito wake.

“msiba huu kwangu ni mzito sio mdogo, naanza maisha ambayo sikuwahi kuyapitia ……niombeeni, maisha magumu sana“ amesisitiza Martine Shigela.

Marehemu Magdalena Layda alizaliwa mwaka 1975, amefariki usiku wa kuamkia Januari 20 mwaka huu, ameacha watoto wawili ambao ni Lorenzo na Loveness na anatarajiwa kuzikwa Kishapu Mkoani Shinyanga Januari 24 mwaka huu.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe. Amina.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.