• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AIPONGEZA TAASISI YA THE ISLAMIC FOUNDATION.

Posted on: November 25th, 2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipongeza Taasisi ya The Islamic Foundation kwa kushiriki masuala ya kijamii na kutoa misaada ya sekta ya Afya, Elimu na Maji ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na kusogeza huduma hizo karibu yao.

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa pongezi hizo Novemba 25, Mwaka huu wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Msikiti Masjid Al Gaith uliopo kata ya Kilakala Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo ujenzi ambao hadi kukamilika kwake utagharimu takribani Tsh. Bil. 7.

Mara baada ya kuweka jiwe la msingi Rais Samia amesema Pamoja na kujenga msikiti huo kwa ajili ya ibada ya waumini wake bado anaipongeza taasisi hiyo kwa kutoa misaada mingi kwa watanzania wote kupitia sekta za Afya, Elimu na Maji.

“… niipongeze Taasisi ya The Islamic Foundation kwa mchango wake kupitia miradi kwenye sekta za afya, elimu na maji, kwa kweli hizi ndio sekta mwenyezi Mungu alizotusisitiza kutoa sadaka…” amesema Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Dkt.  Samia Suluhu Hassan ameiomba taasisi hiyo kuendelea kutoa misaada kwa waathirika wa majanga mbalimbali yanayotokea hapa nchini hususan mafuriko, Matetemeko ya ardhi na njaa ambapo Taasisi hiyo imekuwa kinara wa kutoa misaada kama hiyo. 

Sambamba na rai hiyo, Rais Samia Suluhu Hassan kupitia hafla hiyo amewataka viongozi wote wa dini hapa nchini kuendelea kuhubiri amani, Utulivu na Upendo kwa waumini wao na kuwa kiunganishi ili jamii iweze kuondokana na migogoro isiyokuwa na tija. 

Katika hatua nyingine Rais Samia amesisitiza kuwepo kwa ujenzi wa madrasa ili kuwa na waumini wa kutosha wa kutumia misikiti inayojengwa na kuongeza watanzania wenye hofu ya Mungu kwa kupata elimu sahihi ya dini ndani ya kwa jamii kwa kufanya hivyo kutaendelea kuwa na kizazi chenye maadili mema na kutunza amani na utulivu kwa Taifa.  

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya ndani Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kushiriki kikamilifu katika mialiko ya dini zote jambo ambalo amesema linasaidia kulinda na kutunza amani na utulivu kwa watanzania kwani viongozi wa dini wanafanya kazi kubwa ya kuhubiria maadili yaliyo bora. 

Akitoa salamu za Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Kighoma Malima Pamoja na kumshukuru Rais kwa kuendelea kufanya ziara Mkoani humo amebainisha kuwa msikiti huo utakapokamilika Pamoja na kuwa ni nyumba ya ibada bado utakuwa kivutio kikubwa cha utalii ndani ya Mkoa huo.

Naye, Mwenyekiti wa Taasisi ya The Ilsamic Foundation Sheikh Aref Nadhi amesema Mradi huu unamilikiwa na Taasisi ya The Islamic Foundation ambao unafadhiliwa na jumiya ya Dar Al Ber Society iliyopo Dubai Falme za Kiarabu inayojishughulisha kusaidia kutoa huduma za kijamii Tanzania bara na visiwani hususan sekta ya afya, Maji, elimu, Kulea watoto yatima, Ujenzi wa Nyumba za Ibada, kusaidia waathirika wa majanga na kutoa misaada kwa wasiojiweza.


Msikiti huo utakaogharimu takribani shilingi 7 Bil. Hadi kukamilika kwake, utakapokamilika utakuwa na uwezo wa kuchukua waumini 3000 kwa wakati mmoja.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.