• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AKABIDHIWA OFISI RASMI, AAHIDI KUWEKA MIKAKATI KUUENDELEZA MKOA HUO.

Posted on: June 1st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro mara baada ya kuwasili ofisini hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kushoto) akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kagera wakibadilishana mawazo kabla ya hafla ya makabidhiano rasmi ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Mkoa wa Morogoro una fursa nyingi za kiuchumi ambazo zikitumiwa vizuri uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla utakua.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa (kulia) wakisaini nyaraka za Makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Mhe. Malima ametoa kauli hiyo Juni 1 mwaka huu kwenye hafla ya makabidhiano ya ofisi kati yake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Fatma Mwassa katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema pamoja na Mkoa huo kushika nafasi ya kwanza kwenye uzalishaji wa chakula hapa nchini lakini kuna haja ya Mkoa kuweka mikakati bora ili kuhakikisha kuwa Mkoa huo unashika nafasi ya kwanza kwa uzalishaji wa Chakula.


Mhe. Fatma Mwassa (kulia) akikabidhi nyaraka za serikali kwa Mhe. Adam Malima (kushoto) ikiwa ni ishara ya kukabidhi rasmi ofisi hiyo.

"...tunaenda kujadiliana pale ambapo tunakuwa mtu wa tano au wa nne, kwa nini tusiwe wa kwanza, kinachotukwaza tusiwe mtu wa kwanza ni nini?..." amesema Mhe. Adam Malima.

Aidha, Mhe. Adam Malima amesema mifugo ya Morogoro lazima iwe na mchango kiuchumi ndani ya Mkoa huo na Taifa kwa jumla ndani vinginevyo kitakuwa hakuna maana.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akizungumza na viongozi waliohudhuria hafla ya makabidhiano ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Sambamba na hilo Mkuu huyo wa Mkoa amemuhakikishia Mhe. Fatma Mwassa kuwa ataendeleza mazuri aliyoyaacha katika Mkoa huo pamoja na kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya kuwavutia wawekezaji katika sekta mbalimbali.

Awali, Mhe. Fatma Mwassa ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera amemuhakikishia Mhe. Adam Malima kupata ushirikiano kutoka kwake ili kufanikisha harakati za kuwaletea wanamorogoro maendeleo.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera akitoa taarifa fupi ya Mkoa huo kabla ya kukabidhi rasmi ofisi hiyo.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa huo amemshukuru Mhe. Fatma Mwassa kwa uongozi wake uliotukuka katika kuhakikisha kuwa viongozi ndani ya Mkoa huo wanakuwa na maono ya pamoja.


Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba akitoa neno la shukurani na la ukaribisho kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Morogoro kwenye hafla ya makabidhiano ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.



Picha ya pamoja wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya kiofisi baina ya  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Mkuu wa MKoa wa Kagera. kutoka kushoto waliokaa ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa, Mhe. Adam Kighoma Malima Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Abubakari Mwassa na Mwenyekiti wa CCM MKoa wa Morogoro Joseph Masunga



Hawa ni baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Mkoa wa Morogoro wakiwa katika picha ya pamoja na Wahe. wakuu wa Mikoa ya Morogoro na Kagera baada ya makabidhiano ya kiofisi


Waliosimama ni baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro kushoto ni Alhaji Hamis Sengulo, katikati ni Ndg. Solomon Kasaba na kulia ni Jamila Miyonga wakiwa kwenye picha ya pamoja na wahe. Wakuu wa Mikoa ya Morogoro na Kagera. 


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (wa pili kushoto waliokaa), Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa wakiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa dini wa Mkoa wa Morogoro baada ya hafla fupi ya makabidhiano ya ofisi.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (wa pili kushoto waliokaa), Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro baada ya hafla fupi ya makabidhiano ya ofisi.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (wa pili kutoka kushoto waliokaa), Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa  wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Morogoro.



MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.