• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATAKA VIKUNDI VYA WANAWAKE KUJIKITA KATIKA SHUGHULI ZA KIUCHUMI

Posted on: May 14th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amevitaka vikundi vya wanawake Mkoani humo kujikita katika shughuli za kiuchumi hasa kilimo biashara kwa kuwa mazao mengi ya biashara na viungo yanaweza kulimwa katika maeneo mengi ya Mkoa huo.

Mhe. Malima amesema hayo Mei 14, Mwaka huu wakati akifunga kikao cha kutambulisha Program ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi inayojulikana kama Imarisha Uchumi na Mama Samia ( IMASA ) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Glonency (nanenane) iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kikiwa na lengo la kutoa elimu ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara Wanawake Mkoani humo.

"... mnatakiwa mtengeze kikundi cha watu kumi au zaidi mpate mbegu za kokoa mpande hadi mvune, mkipata Mil. 20 au 30 mtachagua mgawane au muongeze biashara yenu hapo ni nyie wenyewe..."

Aidha, Mhe. Malima amesema shughuli za kiuchumi hasa Kilimo biashara kinaweza kufanyika  katika maeneo mengi ya Mkoa huo ikiwemo Mvomero, Gairo (Nongwe) na Morogoro vijijini (Mvuha) na kubainisha kuwa kilimo kimeongezewa thamani na Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa zao la Kokoa kupanda bei kutoka shilingi 3000 hadi 28000 kwa kila kilo moja.

Katika hatua nyingine, Mhe. Adam Malima amesema kuwapa wananchi fedha  haimaanishi umewasaidia kwani uweshezaji wa kiuchumi ni muhimu kutoa pesa na elimu (maarifa) itakayowasaidia wananchi hususan wanawake kuongoza miradi yao na kuweza kufanya miradi yao kwa uhakika zaidi.

Kwa upande wake,  Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi (NEEC) Bibi Being’i Issa amesema biashara ya uwezeshaji ni muhimu kufanya katika vikundi vilivyosajiliwa na Halmashauri na kutumia vikundi hivyo kuboresha biashara zao.

Sambamba na hilo, Katibu huyo amesema mwaka 2023/2024 kuna mipango mahususi ya kuhakikisha kunapatikana wananchi wengi zaidi wenye hali ya chini kuingia katika manunuzi ya uma, hivyo 30% itatakiwa kwenda kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Naye, Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwekezaji kwa wakina mama wawekezaji Mkoa wa Morogoro Bi. Hadija Mbwana amesema wananchi hasa wanawake wamekuwa wakipoteza fursa nyingi kutokana na uhaba wa mitaji hivyo amesema benki zitaimarisha biashara zao kuleta tija kwao, jamii na Taifa kwa jumla.

Ameongeza kwa kuwashauri wanawake hao kuwa wanapaswa kujiunga kwenye vikundi mbalimbali kisha kuungana na kutengeneza viwanda vidogo vidogo ili kutengeneza ajira za kutosha hivyokujikwamua na umaskini.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.