• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATEMBELEA VIPANDO, ASIFU HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOROGORO NA KIGAMBONI, AZITAKA HALMASHAURI NYINGINE KUKAMILISHA KABLA YA JULAI 29,2023

Posted on: July 22nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam  Malima ametembelea mabanda na vipando vya nane nane ikiwa ni maandalizi ya sherehe za wakulima  na wafugaji maarufu kama  Nanenane kwa Kanda ya Mashariki ambazo zinatakiwa kuzinduliwa  rasmi Agosti 1 mwaka huu katika viwanja vya Julius Kambarage Nyerere na kuwataka washiriki ambao hawajakamilisha maandalizi hayo wakamilishe kabla au ifikapo Julai 29 mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akiwa pamoja na kamati ya maandalizi ya maonesho ya sherehe za nane nane wakati wakikagua mabanda ya Nane nane, hapa walikuwa banda la Halmashauri ya Mji Ifakara.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo Julai 21 mwaka huu wakati akikagua mabanda na vipando hivyo kwa niaba ya Wakuu WA Mikoa mingine ya Kanda ya Mashariki yaani Tanga, Pwani na Dar es Salaam. 

Aidha, Mhe. Adam Malima amefurahishwa kuona baaadhi ya Halmashauri zinazoshiriki sherehe hizo zikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Kigamboni kuonekana zimejiandaa vizuri na kutumia nafasi hiyo kuzihimiza Halmashauri ambazo hazijakamilisha maandalizi hayo kukamilisha kabla au ifikapo Julai 29 mwaka huu.

Hapa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima anaangalia aina za mimea ambayo inafaa na isiyofaa kwa malisho ya mifugo.

“...kwa hiyo tarehe 29 tunatarajia kila mmoja awe ameshafanya mambo yake ili tarehe 30 tuanze maonesho ” amesema Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ( wa pili kushoto) akimsikiliza mtaalam kutoka kampuni ya kuzalisha mbolea aina ya minjingu akielezea namna mbolea hiyo inavyofanya kazi kwa aina mbalimbali za mazao.

Sambamba na hilo, Mhe. Adam Malima amesema Kanda ya Mashariki imekuwa mara zote inafanya vizuri katika maonesho ya Nane nane hivyo amewataka wadau wote wa Kanda ya Mashariki kuendeleza sifa hiyo ya kufanya vizuri.

Hapa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam Malima anaangalia ufugaji wa samaki kwenye banda la Halmashauri ya Manispaa  Kigamboni.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi sehemu  ya Uchumi na Uzalishaji Mali Dkt. Rozalia Rwegasira amesema zaidi ya Taasisi 500 watashiriki katika Maonesho ya mwaka huu ambayo ni sawa na asilimia  mia moja ukilinganisha  na maonesho ya mwaka jana ambapo wadau au Taasisi 400 pekee walishiriki.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (katikati) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebeca Nsemwa (kushoto) kulia ni Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Uchumi na uzalishaji Dkt. Rozalia Rwegasira wakati wakikagua mabanda ya Nane nane.

Aidha, Dkt. Rozalia ameongeza kuwa katika maonesho ya mwaka huu wakulima watajifunza teknolojia ya malisho ya mifugo kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya  wafugaji kukosa malisho ya mifugo wao pamoja na kupata Elimu Bora ya kilimo cha viungo kama Karafuu Pilipili Manga na mdarasini.

Maonesho ya Nane nane 2023 ni maonesho ya  30 tangu kuanzishwa kwake huku kauli mbiu ikiwa ni ”Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula”.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.