• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AWASHUKURU VIONGOZI WA DINI, WANA MOROGORO WOTE

Posted on: November 4th, 2025



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewashukuru wananchi wa Mkoa huo kwa ushirikiano walioutoa kipindi cha kabla, wakati na baada ya zoezi la uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 29 mwaka huu ambapo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha pili cha awamu ya sita.


Mhe. Adam Malima ametoa shukrani hizo leo Novemba 4, 2025 Ofisini kwake wakati akiongea Askofu Mteule wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Morogoro Dkt. George A. Pindua alipofika ofisini kwake kuzungumzia ratiba za uapisho wa Askofu huyo Mteule   ambazo zilikuwa zifanyike tar. 9 Novemba, 2025 hapa Mkoani Morogoro.


Mhe. Adam Malima amesema  katika suala nzima la utulivu, Amani na Usalama uliopatikana ndani ya Mkoa wa Morogoro kabla ya zoezi la upigaji kura, wakati na baada ya wananchi kupiga kura, si la mtu mmoja anayestahili kupongezwa bali pongezi hizo ni za watu wote na wakazi wote wa Mkoa wa Morogoro.


Aidha, Mhe. Adam Kighoma Malima amempongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu kwa kudhibiti hali ya Ulinzi na Usalama ndani ya nchi kwa kipindi chote cha zoezi hilo na kuwezesha leo watanzania kurejea katika shughuli zao za kawaida za kiuchumi na kijamii.


Akipokea pongezi kutoka kwa Askofu Mteule wa KKKT Dkt. George Pindua kwa kuuweka Mkoa katika hali ya Utulivu na Amani, Mhe. Malima ametumia fursa hiyo kutoa shukrani zake kwa Viongozi wote wa Dini na madhehebu mengine walioko ndani ya Mkoa huo kwa ushirikiano na kazi kubwa waliyoifanya ya kuhubiri Amani, Upendo na Utulivu na kumwomba afikishe salam hizo za shukrani kwa viongozi wenzake wa Dini wa Mkoa huo.


Pia shukrani hizo amezipeleka kwa makundi mbalimbali wakiwemo wazee akinababa,Vijana, wafanya biashara, wakulima na wafugaji pamoja na wanahabari ambao wote kwa pamoja wamefanya kazi kubwa ya kuelimisha jamii si juu ya umuhim wa kupiga kura tu bali pia kupiga kura kwa Amani na utulivu.


Mkuu wa Mkoa hakuyasahau makundi ya mama lishe, baba lishe, machifu wa maeneo mbalimbali ya Morogoro, wamachinga, Asasi zisizo za Kiserikali, bodaboda madereva wa magari makubwa ya mizigo, mabasi, madereva wa daladala na bajaji na wote ambao hajawataja bila kukusudia lakini nao amewataka wapokee  pongezi hizo.


Amesema, makundi hayo yote yamechangia kwa kiasi kikubwa katika kuuweka Mkoa huo katika hali ya utulivu ambapo hadi sasa upo shwari na wananchi wake wanaendelea na kazi zao za kila siku kwa amani na utulivu. Na kuendelea kuabudu katika nyumba zao za ibada bila mashaka.


Hata hivyo pongezi za shukrani amezielekeza kwa Kamati yake ya Ulinzi na Usala ya Mkoa, KUU Wilaya Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya, Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata, Vijiji/Mita na watumishi wote wa Umma ndani ya Mkoa huo na Taasisi zote za Serikali.


Naye Askofu huyo Mteule wa KKKT Dayosisi ya Morogoro amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa ushirikiano anaouonesha tangu alipoanza kuuongoza Mkoa wa Morogoro lakini pia kwa kipindi hiki cha maandalizi ya zoezi la kupiga kura ambapo aliwaalika katika vikao mbalimbali vilivyohusu mstakabali wa upigaji kura na kwamba hiyo ndio imechangia sana kuleta utulivu. Wa mkoa.


Katika hatua nyingine mazungumzo ya Mkuu wa Mkoa Adam Kighoma Malina na Askofu Mteule George Pindua yalihusu KUAHIRISHWA KWA IBADA YA KUINGIZWA KAZINI KWA ASKOFU MTEULE DKT. GEORGE A. PINDUA  PAMOJA NA MSAIDIZI WAKE  MCH. PETER MICHAEL MAKALLA.


Hafla hiyo ya Kuingizwa kazini Askofu Dkt. George Pindua iliyopangwa kufanyika Tarehe 9 Novemba, 2025, kwa sababu zisizozuilika imeahirishwa  hadi tarehe 14 Disemba, 2025.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AWASHUKURU VIONGOZI WA DINI, WANA MOROGORO WOTE

    November 04, 2025
  • KUELEKEA UCHAGUZI MKUU, RC MALIMA ASEMA MOROGORO IKO SHWARI, AHIMIZA WANANCHI WALIOJIANDIKISHA KWENDA KUPIGA KURA

    October 28, 2025
  • Morogoro kuimarisha ushirikiano na Zanzibar katika nyanja ya kilimo

    October 16, 2025
  • Morogoro kuanzisha jarida la programu ya PJT–MMMAM

    September 30, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.

  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • AERO88
  • YAMITOTO
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • YAMITOTO
  • Toto Slot Gacor
  • AXL777
  • AERO88
  • AXL777
  • Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Slot Gacor
  • Situs Toto Online
  • Situs Toto
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • UFABET
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200