• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima awataka Wakurugenzi wa Halmashauri Kutenga Maeneo ya Uwekezaji

Posted on: February 20th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro zilizo karibu na hifadhi za Taifa kutenga maeneo maalum isiyo na migogoro na yenye usalama kwa ajili ya uwekezaji.


Mhe. Malima ametoa agizo hilo Februari 20, Mwaka huu, katika Mkutano wa Wawekezaji wa Mkoa wa Morogoro uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Cate Hotel iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.


Akifafanua zaidi, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa wawekezaji wakubwa huvutiwa na miundombinu bora kama vile barabara, viwanja vya ndege na usalama wa maeneo husika, hali inayoweza kuchochea kirahisi ujenzi wa hoteli za kisasa kwa ajili ya watalii.


Katika hatua nyingine, Mhe. Malima amewataka wawekezaji wa Mkoa wa Morogoro kuwa wabunifu na kuzalisha bidhaa, huduma na mazao yenye ubora wa juu kwani Mkoa huo una rasilimali nyingi zinazotosheleza mahitaji makubwa ya uwekezaji.


Hivyo kuongeza kuwa wawekezaji kuwekeza katika maeneo yanayozunguka hifadhi kutokana na ongezeko la watalii katika Mkoa huo baada ya watalii wengi kuongezeka kwa sababu ya uwepo wa Reli ya SGR, viwanja vya ndege na barabara, kuongeza mapato ya fedha za kigeni na kukuza uchumi wa nchi.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Dkt. Binilith Mahenge, amesema Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa Mikoa bora kumi kuwa na idadi ya miradi ya uwekezaji ambapo Mkoa huo ni wa saba na una miradi 22 ya uwekezaji yenye thamani ya Dola za Marekani 447.5.


Mwaka 2024, Kituo hicho cha uwekezaji cha TIC kilikadiria Mkoa huo kuwa na idadi ya miradi 45 ya uwekezaji lakini hadi sasa Mkoa huo una miradi 22 ya uwekezaji iliyosajiliwa, ikiwemo miradi ya kilimo, viwanda, utalii na usafirishaji.


Naye, Meneja wa TIC Kanda ya Mashariki, Bi. Grace Lemunge, amesema kuwa kikao hicho kinalenga kuwaelimisha wawekezaji kwa kuwapatia taarifa kuhusu fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika Halmashauri za Mkoa wa Morogoro.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.