• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MWASSA AUNDA KAMATI KUHAKIKI UPIMAJI ARDHI.

Posted on: February 18th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe.  Fatma mwassa  ameunda kamati ya watu 5  ambao watashirikiana na kamishna wa ardhi wa Wilaya ya Mvomero na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuhakiki na kupima eneo lenye ekari  5,000 ambalo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliagiza eneo hilo kugawanywa kwa wananchi waishio eneo hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika eneo la msitu wa kuni wa CCT.

Mhe. Fatma Mwassa ameunda Kamati hiyo Februari 18 mwaka huu wakati wa  mkutano wa hadhaara na wananchi waishio eneo la msitu wa kuni wa CCT Wilayani Mvomero Mkoani Moroggoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema ameunda kamati hiyo ambayo wajumbe wake ni wananchi waishio katika eneo hilo lengo kuu la kuwashirikisha wananchi hao ni kuhakiki na kupima ekari hizo 5,000 ili kuondoa utata ambao unaweza kujitokeza baadae.

wajumbe wa kamati iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa kwa lengo la uhakiki upimaji ardhi kwenye eneo la ekari 5,000 wakiwa wamesimama mbele ya hadhara kwa ajili ya utambulisho.

“...na sasa tuna kamati, na hii itatusaidia sana kwenye kutatua changamoto...” amesema Mhe. Fatma Mwassa.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ameiagiza TFS kwenda kung’oa mahindi yao katika eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya uhifadhi wa msitu huo kutokana na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi wa eneo hilo.

Wananchi wakiwasikiliza viongozi  mbalimbali kwenye mkutano wa hadhara katika eneo la msitu wa kuni CCT Wilayani Mvomero.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewataka wananchi kutoa kero zao bila woga mbele ya viongozi wao pindi wanapo watembelea ili kutatua kero na changamoto zinazowakabili.

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli akitoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa na wananchi waliodhuria mkutano huo.

Awali, Bwana Denis Leo mkazi eneo hilo ameilalamikia TFS kwa kuwaondoa katika eneo la hifadhi na wao kulitumia eneo hilo kwa ajili ya kilimo jambo ambalo tayari Mhe. Mkuu wa Mkoa amekwisha litolea maelezo na maelekezo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.