• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SACCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU, KUZINGATIA VIWANGO VYA KIMATAIFA.

Posted on: November 21st, 2023

Mkurugenzi wa fedha na utawala CPA Prisilla Mushi amewasisitiza watendaji wa Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) kuwa wabunifu katika kazi zao kwani amesema kumekuwa na mashirika mengi ya ukopeshaji na utoaji huduma za fedha ikiwemo VIKOBA, na kuwataka kuwa na utendaji unaolenga viwango vya kimataifa ili kuwa na mwendelezo mzuri kwa wateja wao na kuongeza wateja zaidi.

CPA Mushi ametoa kauli hiyo Novemba 21, 2023 katika mafunzo ya watendaji wa SACCOS kuhusu masuala ya uhasibu na ukaguzi yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Nashera iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo watendaji hao.

”... sasa hivi taasisi nyingi zinapambana kupata deposit kama vikoba naona mnakuja juu sana kwa hiyo SACCOS mnatakiwa kuwa wabunifu katika utendaji ili kuendana na viwango vya kimataifa...”

Katika hatua nyingine, CPA Mushi amewataka watendaji hao kufuata utaratibu katika kuchukua hati ili kuwa na hati safi ambapo amebainisha kuwa mwaka 2022 hati safi zilikuwa 23% na mwaka 2023 zimekuwa 28.2% huku akibainisha kuwa hati hizo haziridhishi ambapo changamoto kubwa ikiwa kutofuata utaratibu mzuri na kupata hati safi, hivyo mafunzo hayo yatakuwa mwarobaini wa kutibu tatizo hilo.

Kwa upande wake, Kaimu meneja kitengo cha ushauri COASCO CPA. Gabriel Msuya  amesema kuwa kitengo hicho kimefanya utafiti na kugundua kuwa baadhi ya watendaji wanakwama kutokana na tatizo la uelewa hasa kwenye kufuata taratibu, kanuni na sheria zote za  kupata hati safi, hivyo mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha watendaji hao kupata uelewa wa pamoja ili kuondoa changamoto hiyo.

Naye Mshiriki wa mafunzo hayo wa URA SACCOS LTD kutoka Dar es salaam kwa niaba ya washiriki wote amesema kumekuwa na changamoto kubwa katika Vyama vya Ushirika hasa katika hesabu zinazoendana na viwango vya kimataifa hivyo mafunzo hayo anaamini yataboresha utendaji wao wa kazi.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.