• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

TUHAKIKISHE WAWEKEZAJI WETU TUNAWALINDA - MHE. MWANYIKA.

Posted on: February 20th, 2025



Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifubo, Mhe. Deo Mwanyika (MB) amewahakikishia wawekezaji wa ndani kuvilinda viwanda vyao na kuagiza Uongozi wa kiwanda cha sukari cha Kilombero kuanza uzalishaji wake wa sukari bila hofu yoyote.

Mwenyekiti huyo amebainisha hayo Februari 19 mwaka huu akiwa katika kiwanda cha sukari cha Kilombero Mkoani Morogoro yeye na wajumbe wa Kamati hiyo wakiendelea na ziara yao ya siku sita Mkoani humo ikiwa leo ni siku yao ya tano ya ziara hiyo.

Mhe. Mwanyika amesema kuna umuhimu mkubwa wa Serikali kuwalinda wawekezaji wa ndani pia kulinda viwanda vya ndani ili kuleta chachu ya uzalishaji wa bidhaa ili nchi iweze kusafirisha bidhaaa hizo katika nchi mbalimbali.

"..Lazima tuhakikishe kwamba wawekezaji wetu tunaendelea kuwalinda " Amesema Mhe. Deo Mwanyika.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde (MB) amesema Serikali imejizatiti kuwalinda wawekezaji wazawa kwa kuwekeza na kuongeza thamani ya mazao yanayolimwa hapa nchini kwani amesema hiyo ndiyo sera ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali yake na kwamba kwa kufanya hivyo tutaondokana na umaskini na kwenda katika hatua nyingine ya kiuchumi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema kwa Mkoa wa Morogoro uzalishaji wa Mpunga ni chini ya Tani 1000,000 hivyo Serikali inaendelea kuboresha maiundombinu kwa kuwavutia wawekezaji wa zao la mpunga kuwekeza ili kuongeza tija ya zao hilo na  kuongeza uzalishaji wa zao hilo la mpunga,

Pia Mhe. Malima amemshukuru mwekezaji wa kiwanda kidogo cha kuchakata mpunga kwa kuweza kutoa ajira kwa watoto waliozaa mapema ambapo ni moja ya maono ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rias wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuhakikisha wanawake hao wanawezeshwa kiuchumi.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.