• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda ahimiza vikundi kuchukua mikopo

Posted on: August 8th, 2024

Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda amevitaka vikundi mbalimbali vya Vijana, akina mama na makundi maalum kuchukua mikopo ya asilimia 10 ili kuongeza mitaji hivyo kuwa na uzalishaji wenye tija.

Mhe. Mizengo amesema hayo Agosti 8, mwaka huu wakati wa kilele cha maonesho ya siku ya wakulima maarufu kama Nanenane kanda ya mashariki yaliyofanyika katika viwanja vya Mwl. Julius Kambarage Nyerere vilivyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro yakiwa na lengo la kutoa elimu na kuwajengea uwezo wakulima, wafugaji na wavuvi.

Waziri Mkuu Mstaafu huyo amebainisha vikundi hivyo kuwa ni vile vinavyojihusisha na kilimo,ufugaji na uvuvi kuchukua mikopo hiyo ili kuongeza mitaji yao na kuzalisha kwa tija.

"... tumevikuta vikundi viko hali ya juu kiuchumi lakini vimetokana na mfuko wa 10% na vingine vinapaswa kuchukua kutekeleza majukumu yao, Wakurugenzi wa Halmashauri waliangalie hilo..." Amesema Mhe. Peter Pinda

Akifafanua zaidi, Mhe. Pinda amesema Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri wanatakiwa kuibua vikundi vitakavyonufaika kutokana  na mikopo hiyo ili kuendana na kasi ya kiteknolojia katika uzalishaji wa mazao ya Kilimo, ufugaji na uvuvi.

Aidha, Mhe. Pinda amesema kilimo, ufugaji na uvuvi umesaidia kupunguza tatizo la ajira hapa nchini kwani vijana wamekuwa wakifanya shughuli hizo kama vyanzo vikubwa vya kuwaingizia kipato.

Waziri Mkuu huyo mstaafu amehimiza umoja na mshikamano ndani ya kanda hiyo kwani ina rasilimali watu zaidi ya Mil. 13 sawa na 21.4% ambapo Dar es salaam ina watu Mil. 5, Morogoro ina watu Mil. 3, Pwani ina watu Mil. 2 na  Tanga - mil 2.6 ambao ndio chanzo cha uzalishaji mali katika shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi. 

Katika hatua nyingine, Mhe. Mizengo Pinda amewataka wananchi kula mlo kamili hususan vyakula vya aina ya mboga mboga kuepuka matatizo ya kiafya ukiwemo ugojwa wa utapia mlo ambao husababishwa na kula vyakula bila kujali lishe.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima   amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika ushiriki wa maonesho ya Nane Nane kanda ya mashariki 2024 kutokana na kuwepo kwa ubunifu wa kiteknolojia katika sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi, ambapo yamefanya maonesho hayo kuvutia zaidi hapa nchini.

Pia Mhe. Malima amesema Kanda hiyo inapaswa kutumia fursa ya ardhi iliyopo kwa ustadi ili kujipatia chakula cha kutosha, huku akihimiza maonesho hayo kuwa ya vitendo zaidi kwa kile kinachooneshwa na wataalam ndani ya viwanja vya Nanenane vikafanyike maeneo wanakofanyia kazi.

Hata hivyo,  Mkuu huyo amewataka wafugaji na wakulima kuwa mfano hapa nchini, kuishi kwa amani na kuheshimiana na kuwataka wafugaji kuwa na maeneo yao ya kulishia mifugo ili kuondoa migogoro isiyo kuwa na tija hapa nchini.

Maonesho ya nanenane hufanyika kila mwaka kuanzia Agosti 1 hadi 8 ambapo mwaka huu yamekuwa na kaulimbiu inayosema " Chagua viongozi bora wa Serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya Kilimo, mifugo na uvuvi"



MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.