• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Baraza la Madiwani Morogoro watakiwa kubuni vyanzo vya mapato

Posted on: December 11th, 2020

Baraza la Madiwani Morogoro latakiwa kubuni vyanzo vya mapato

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro limeshauriwa  kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuifanya Halmashauri hiyo kujiendesha yenyewe badala ya kutegemea fedha kutoka Serikali Kuu,

Ushauri huo umetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo wakati akizindua Mkutano wa  kwanza wa Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo uliofanyika Disemba, 11 mwaka huu katika Makao Makuu ya Halmashauri yaliyoko Mvuha.

Mhandisi Kalobelo amesema, Halmashauri hiyo ina vyanzo vingi vya mapato ambavyo bado havijaibuliwa na una maeneo makubwa na mazuri yaliyoiva kwa uwekezaji, hivyo amewataka Madiwanai watumie fursa hiyo kwa ajili ya kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuifanya Halmashauri hiyo kusonga mbele.

“Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro sio Mvuha peke yake, tunaweza kutumia eneo ambalo ni tayari limekwisha iva kwa uwekezaji. tubuni, tutaishi maisha kana kwamba tuko Manispaa”  alisema Mhandisi Kalobelo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo

Amesema eneo lote la ukanda wa Mkambarani na Bwawani ni nzuri kwa uwekezaji na kwamba kinachotakiwa ni nia thabiti, maamuzi na kwamba ana amini Baraza lililoingia madarakani sasa litajikita katika kutafuta njia za kujitegemea kimapato na si kulia lia. 

Katika hatua nyingine Mhandisi Kalobelo amelitaka Baraza hilo la Madiwani kujiepusha na Mabishano yasiyo na tija katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo, kwa kuwa amesema mabishano hayo yanaicheleweshea Halmashauri kujiletea maendeleo badala yake amewataka kujikita katika kuwaletea wananchi maendeleo. Mhandisi Kalobelo alihitimisha hotuba yake kwa kuwataka Madiwani kuanza kazi ya kuwatumikia wananchi kwa kuanza na kutekeleza agizo la Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, la kuhakikisha ifikapo Februari 28 wananfunzi wote wawe madarasani wanasoma wakiwa wamekalia madawati, na kwamba hilo ni agizo la Serikali, halijadiliwi lazima litekelezwe. 

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mhe. Innocent Kalogeresi akiwa katika kikao cha Madiwani

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki Mhe. Tale Tale, alishiriki kikamilifu mkutano huo

Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Bakari Msulwa, amewataka Madiwani wa Halmashashauri hiyo kila mmoja kuainishi shule ambazo zina upungufu wa madawati na wana misitu ili kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri na uongozi wote wa Halmashauri kuomba kibali cha kukata miti katika Wilaya hiyo kwa ajili ya kutengeneza madawati ya wanafunzi ili ifikapo Februari 28 mwakani wanafunzi wote wa shule zilizopo katika Wilaya ya Morogoro wawe katika mazingira mazuri ya kusomea kwa lengo la kutekeleza agizo la Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

kushoto, ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amewapongeza Wabunge wa Majimbo ya Morogoro Kusini Mhe. Innocent Kalogeresi na wa jimbo la Morogoro Kusini Mashariki Mhe. Tale Tale kwa ushindi walioupata huku akibainisha kuwa mipango yao ambayo wameanza kuipanga ina nia ya kuwaletea maendeleo wananchi wao.

Ruth John ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, ndiye alikuwa Mwenyekiti wa muda wa Mkutano huo wa kwanza wa Baraza la Madiwani.Hapa Mwenyekiti wa muda Ruth John (kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashaur hiyo moja ya vitendea kazi vyake, joho ambalo huvaliwa rasmi wakati wa vikao vya wahe. Madiwani

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Rehema Bwasi, ambaye katika Mkutano huo alikuwa ni katibu wa kikao, akitoa miongozo mbalimbali kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mhe. Lucas Lemomo wa kutoka Kata ya Matuli ambaye amechaguliwa kwa kura zaidi ya tisini kukalia kiti hicho, kwa niaba ya Madiwani wenzake ameahidi kuvunja makundi yaliyokuwepo hapo awali ambayo yaliyakuwa yanachelewesha maendeleo ya Halmashauri hiyo huku akiahidi kuyafanyia kazi maagizo ya Katibu Tawala wa Mkoa Morogoro Mhandisi Emmanueli Kalobelo hususan katika suala nzima la kubuni vyanzo vipya vya mapato vya Halmashauri ili kuhakikisha Halmashauri hiyo inajiendesha yenyewe.

MHuyu ndiye wenyekiti mpya wa Halmashauri ya wilaya ya Morogoro Mhe. Lucas Lemomo

Maafisa Kutoka Sekretarieti ya Mkoa, Idara ya Serikali za Mitaa, walishiriki Kikao cha Madiwani katika kuhakikisha kuwa uchaguzi wa Viongozi wa Baraza hilo unafuata Sheria,Taratibu na kanuni. kutoka Kushoto ni Christer Njovu na Marcelin Ndimbwa

Naye Diwani wa Viti Maalum wa Kata ya Bwakila Mhe. Asha Nyakaema alieleza namna kata yake inavyoshirikiana na wananchi wake katika kuendeleza Sekta ya Elimu hususana katika kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati na vyumba vya madarasa.

Baadhi ya Wahe. Madiwani wakiwa katika Mkutano wao wa kwanza

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.