• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MWENGE WA UHURU WAMULIKA MIRADI YA THAMANI YA ZAIDI YA BIL 1.5 IFAKARA MJI

Posted on: April 26th, 2024


MWENGE WA UHURU WAMULIKA MIRADI YA THAMANI YA ZAIDI YA BIL 1.5 IFAKARA MJI


Mwenge wa Uhuru umendelea kukimbizwa Mkoani Morogoro tangu ulipowasili Aprili 20, 2024 hadi leo Aprili 26, 2024 umekwisha pitia miradi ya maendeleo mbalimbali katika Halmashauri saba kati ya Halmashauri Tisa za Mkoa wa Morogoro.

Leo Aprili Aprili 26, 2024 Mwenge wa Uhuru umekimbizwa katika Wilaya ya Kilombero Halmashauri ya Ifakara Mji na Kupitia miradi ya maendelep Nane yenye thamani ya Shilingi Bil. 1,586,216774.50.

Mchanganuo wa fedha hizo ni kama ifuatavyo: nguvu za wananchi shilingi 23,600,000.00, Halmashauri shilingi 85,568700.00, Serikali Kuu 637949954.50 na wahisani au wadau wengine wa maendeleo wamechangia shilingi 839,098120.00

Moja ya miradi ya maendeleo iliyotembelewa ni Pamoja na uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Mhelule kilichopo Tarafa ya Mang’ula wilayani kilombero Mkoani Morogoro wenye gharama ya shilingi 542,989,954.5 baada ya kupata fedha kutoka mfuko wa Maji wa Taifa – NWF na utanufaisha wakazi wapatao 2,838

Akiwa katika eneo hili Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Godfrey Mnzava alisitiza na kuwataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa huo kuandaa program maalum ya kuwawezesha Wajumbe wa Kamati ya     Ulinzi na Usalama (KUU) ngazi ya Wilaya ili waweze kuelewa vema mfumo wa NeST unavyofanya kazi jambo litakalowarahisishia wajumbe hao kufuatilia mfumo huo kufanya kazi inavyotakiwa na hivyo kutoa matokeo Chanya na yanayotarajiwa na Serikali.


Katika hatua nyingine Mwenge huo wa Uhuru uliona shughuli za utunzaji mazingira zinazofanyika kando ya mto Lumemo unaopita katikakati ya Mji wa Ifakara ambapo kulikuwa na kampeni ya kupanda miti takribani wiki moja na kufanikiwa kupanda miti 2000. Mwenge wa Uhuru nao ulifanikiwa kufika katika eneo hilo na kushirikiana na wananchi wa Mji wa Ifakara kupanda miti 1000 hivyo kufanya jumla ya miti iliyopandwa kufikia miti 3000.

Ujumbe wa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa wananchi sio kupanda miti tu, bali kupanda miti 1,500,000 kila mwaka kama maagizo ya Serikali ambavyo yalishatolewa lakini zaidi ni kutunza miti hiyo ikue na kuleta mafanikio tarajiwa ikiwa ni Pamoja na kupunguza chanagamoto ya mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni Pamoja na mafuriko ambayo yamekithiri pahala pengi duniani.

Mradi mwingine uliotembelewa ni Pamoja na Uzinduzi wa Ukumbi wa Mikutano kutoka Sekta binafsi ambapo amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira mazuri ya wawekezaji binafsi wa ndani na nje ya nchi ili kushirikiana katika kulijenga taifa hili.

 Aidha amemshukuru Mwekezaji wa Mradi huo kwa kuwa anachangia pato la Serikali kwa kulipa kodi mbalimbali za shughuli yake lakini pia kupitia uwekezaji wa mradi huo kwa vyovyote ametoa ajira kwa watanzania wenzake.


MWISHO



Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.