• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAIS SAMIA AWATAKA WAFANYAKAZI KUWA WAADILIFU, KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

Posted on: May 1st, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka Wafanyakazi wa Sekta zote hapa nchini kufanya kazi kwa Weledi na kuwa waadilifu katika utendaji wao kazini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia  Viongozi, Wafanyakazi na wananchi kwenye kilele cha Maadhimisho ya Sherehe za Mei Mosi Kitaifa ambayo yamefanyika katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.

Rais Samia ameyasema hayo Mei 1 mwaka huu wakati akihutubia Viongozi, Wafanyakazi na Wananchi kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) ambayo Kitaifa yamefanyika katika Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.

Viongozi mbalimbali wa Serikali na taasisi nao wameudhuria Maadhimisho ya Sherehe za Mei Mosi Kitaifa ambayo yamefanyika katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.

Dkt. Samia amesema pamoja na Wafanyakazi hao kudai maslahi yao ya kazi bado wanatakiwa kuwa  waadilifu na kufanya kazi kwa weledi katika kutekeleza majukumu yao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wakiimba wimbo wa mshikamano (Solidarity) kwenye Maadhimisho ya Sherehe za Mei Mosi Kitaifa 2023 katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

“...kwa hiyo pamoja na kudai mishahara bora, lakini uadilifu na weledi kazini ndio utaleta maisha bora kwa wafanyakazi...”. amesema Rais Samia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akigawa zawadi kwa wafanyakazi bora pamoja na washindi wa michezo ya Mei Mosi.

Sambamba na hilo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewahakikishia wafanyakazi kuwa Serikali itaendelea kuboresha na kuimarisha mazingira ya kazi ikiwemo, kuwapandisha madaraja wafanyakazi, kuwaongezea mishahara na posho za wafanyakazi.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema kutakuwa na nyongeza za mishahara kwa wafanyakazi ambayo itakuwa inaongezeka kwa kila mwaka, nyongeza hiyo inatarajia kuanza mwaka huu 2023.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. FatmaMwassa akiwa kwenye picha ya pamoja Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Morogoro akiwemo Mhe. Sebastian Waryuba Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Mhe. Judith Nguli Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Shaka Hamdu Shaka Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Danstan Kyobya, Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Mhe. Dkt. Julius Ningu, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame na Mhe. Rebeca Nsemwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa wakati akitoa salam za Mkoa, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi kubwa zinazofanywa katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Mhe. Fatma Mwassa ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Samia wafanyakazi Mkoani Morogoro wameboreshewa maslahi yao ikiwemo kupandishwa madaraja takribani wafanyakazi 7108 wamepandishwa madaraja, 2030 wameajiriwa kwa sasa Mkoa umepata kibali cha kuajiri wafanyakazi 3891 wa kada mbalimbali pamoja na kuongeza mishahara.

Nae Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya ameishukuru Serikali sikivu ya Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali wafanyakazi wake kwa kuwaboreshea mazingira na maslahi yao ya kazi, kulipa2 madai yao, kupandisha vyeo watumishi, pamoja na kuwaongezea mshahara.

Maadhimisho hayo ya Mei Mosi kwa Mwaka huu yanaenda sambamba na kaulimbiu isemayo “Mishahara bora na ajira ni nguzo kwa maendeleo ya wafanyakazi, wakati ni sasa”.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.