• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro awataka Viongozi waSerikali kujitathmini utekelezaji wa mkataba wa Lishe.

Posted on: June 3rd, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa akizungumza na wadau wa Lishe waliohudhuria kikao hicho.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Musa Ali Musa amewataka watendaji wa Serikali Mkoani Morogoro hususan maafisa lishe kujitathmini kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Lishe na kuhakikisha wanautekeleza Mkataba huo kwa mujibu wa Mkataba pasi na kukwepesha fedha zinazotolewa kwa ajili hiyo.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Utawala na Rasilimali watu Bw. Herman Tesha (kulia), Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Kusirye Ukio (katikati) pamoja na Bw. Steven Benedict Mkaguzi wa Ndani Mkoani Morogoro wakati wa kikao cha tathmini ya Mkataba wa lishe.

Dkt. Mussa Ali Mussa amesema hayo juni 2, 2023 wakati wa kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe ngazi ya Mkoa kwa kipindi cha januari - machi mwaka huu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

"Kwa hiyo sisi wenyewe tuanze kujitathmini...kila anayejiona amewekewa alama nyekundu, njano au nyeupe muanze kuchukua hatua kama hii niliyochukua mimi..." Amesema.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro wakiwa kwenye kikao.

Dkt. Musa amebainisha kuwa Mkoa huo haufanyi vizuri suala la lishe kutokana na baadhi ya watendaji ngazi ya Wilaya kutokuwa na umakini katika kutekeleza mkataba huo na kuwataka viongozi wao kupambana na uzembe unaojitokeza kwani Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anadhamira ya dhati na Afya za watoto na kwa jamii nzima kwa ujumla.

Sambamba na maagizo hayo, amewashauri watendaji hao kujikita katika kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora ili kuondokana tatizo la udumavu wa akili na mwili, kwani madhara ya kukosa lishe bora hupelekea kudumaa, Ngozi kusinyaa, utapiamlo, kwashakoo na matatizo mengine mengi.

Kwa upande wake, Afisa lishe Mkoa wa Morogoro Bi. Salome Magembe amewaomba watendaji ngazi ya jamii ambao nao walisaini mkataba wa lishe wanatakiwa kushirikiana vema na halmashauri kupeleka huduma za chakula mashuleni kwa kuzingatia watoto wote badala ya kutoa chakula hicho kwa madarasa machache.

Afisa Lishe Mkoa wa Morogoro Bi. Salome Magembe akiwasilisha hali ya lishe ya Mkoa huo.

Aidha, amesisitiza kutoa Elimu ya lishe kwa wazazi au walezi na ndugu kushirikiana na serikali katika kutoa chakula kwa watoto mashuleni kwani chakula kinachotumika shuleni kwa mtoto ni kile kile ambacho kingetumika kwa mtoto huyo wakati akiwa nyumbani.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Uchumi na uzalishaji Dkt. Rozalia Rwegasira (kushoto) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Morogoro Mhe. Rehema Bwasi wakati wa kikao.

Mwisho.



Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.