• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro azindua kampeni kuhamasisha utoaji wa chakula shuleni kwa kutumia vyakula vya asili.

Posted on: January 20th, 2024

RAS Morogoro azindua kampeni kuhamasisha utoaji chakula shuleni kwa kutumia vyakula vya asili.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amezindua kampeni ya kuhamasisha utoaji wa chakula cha mchana kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Mkoani Morogoro kwa kutumia vyakula vya asili vinavyopatikana Mkoani humo.

Dkt. Mussa Ali Mussa amezindua kampeni hiyo Januari 19, 2024 katika viwanja vya shule ya msingi Mtombozi iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kwa lengo la kuhamasisha wazazi na walezi kuchangia upatikanaji wa chakula cha mchana kwa wanafunzi Mkoani.

Dkt. Mussa mesema, Mkoa huo umebarikiwa kuwa na aina mbalimbali za vyakula vya asili vikiwemo mashelisheli, mihogo, Viazi vitamu na ndizi huku akisema kuwa haoni sababu ya wanafunzi kukosa chakula cha mchana na kuwataka wazazi kwa kushirikiana na Walimu kufanikisha upatikanaji wa vyakula hivyo kulingana na maeneo husika.

“...kuja kwangu leo hapa ni kuanzisha hii kampeni, si kwa hapa tu lakini kwa Halmashauri nzima na Morogoro nzima lazima tukubali kutumia vyakula vyetu vya asili tulivyokuwa navyo...” amesema Dkt. Mussa.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameongoza Viongozi, wazazi na wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kupata chakula cha asili mara baada ya uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha utoaji wa chakula shuleni kwa kutumia vyakula vya asili.

Aidha, Katibu Tawala huyo ameeleza kuwa kukosekana kwa chakula cha mchana kuna sababisha utoro na kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi. Pamoja na uzinduzi wa kampeni hiyo ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kuhakikisha kuwa inapanda miche ya mashelisheli angalau miche miwili kwa kila shule zote Wilayani humo.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa akipokea zawadi ya vyakula vya asili vikiwemo Mashelisheli, Ndizi, Magimbi na Mihogo kutoka kwa Diwani Kata ya Mtombozi Mhe. Yahaya Mfaume kwa niaba ya wananchi wa kata hiyo.

Naye Afisa Lishe Mkoa wa Morogoro Bi. Salome Magembe amewashauri wazazi na walezi kuzingatia makundi matano ya vyakula Vikiwemo vyakula vya protini, wanga, Vitamini, mafuta na mboga mboga ili kupata mlo kamili kwa ajili ya kuboresha afya za watoto wao.

Afisa lishe Mkoa wa Morogoro Bi. Salome Magembe akifafanua kuhusu umuhimu wa lishe kwa kuzingatia makundi matano ya chakula wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha utoaji wa chakula shuleni kwa kutumia vyakula vya asili.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro amemshukuru Katibu Tawala huyo kwa kuzindua kampeni hiyo ambayo itasaidia kupandisha kiwango cha ufaulu katika Halmashauri na kumhakikishia kuwa watatekeleza maagizo aliyoyatoa.

Katika kuhamasisha kampeni hiyo Dkt. Mussa ameahidi kuichangia shule ya msingi Mtombozi dagaa kilo 100 kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi wa shule hiyo.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio amewataka wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro na Mkoa huo kuchukua taadhali ya ugonjwa wa kipindupindu ambao umekuwa tishio hapa nchini.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.