• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AAGIZA TAKUKURU KUCHUNGUZA MRADI WA UMWAGILIAJI MGONGOLA.

Posted on: March 3rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani humo pamoja na vyombo vingine vya usalama kuchunguza maendeleo ya mradi wa skimu ya umwagiliaji wa Mgongola iliyopo Wilayani Mvomero ili kujua ukweli wa sababu zinazopelekea mradi huo kutokamilika.


Mhe. Adam Malima ametoa agizo hilo leo Machi 3, 2025 wakati wa kikao cha kujadili hali ya mradi huo wa umwàgiliaji, kikao ambacho kimehusisha uongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya, Wizara ya Kilimo pamoja na Mkandarasi anayetekeleza mradi huo ambaye ni M/S BADR EAST AFRICA ENTERPRISES LIMITED kikiwa na lengo la kutatua changamoto za mradi huo.

Amesema, TAKUKURU inapaswa kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini changamoto ya kutokamilisha mradi huo iko upande gani kati ya wataalam wa serikali na mkandarasi anayetekekeza mradi ili kunusuru fedha za Serikali kutotumika ipasavyo badala yake mradi huo ukamilike na kuwaletea faida wananchi kama Serikali ilivyokusudia.

"...TAKUKURU, uhamiaji na vyombo vingine vya usalama nendani na hawa mabwana mkafanye uchunguzi halafu mje na majibu ili tutatue hili jambo..." ameagiza Mhe. Malima.


Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde (MB) aliyeshiriki kikao hicho mwanzo hadi mwisho sambamba na maagizo hayo ya Mkuu wa Mkoa amesema Serikali haiwezi kufurahishwa na maumivu na kodi ya watanzania kwa sababu ya mtu mmoja na kuathiri watanzania walio wengi.


Aidha, Mhe. Silinde amesema Serikali ina nia njema na wananchi wake hivyo mkandarasi anapaswa kufanya kazi kwa ushirikiano na watendaji wote wa serikali ili kufanikisha mradi huo kwani amesema kufanya kazi kinyume na mkataba kunaongeza gharama za mradi na kuathiri manufaa ya mradi kwa wananchi na muda wa mradi kukamilika.


Mradi huo ambao kwa mujibu wa mkataba hadi kukamilika kwake utagharimu Shilingi Bilioni 5.6, unajengwa na mkandarasi M/S BADR EAST AFRICA ENTERPRISES LIMITED tangu mwaka 2022 bila kukamilika na kusababisha malalamiko kutoka kwa wananchi wa Wilaya ya Mvomero ambao ndio wanufaika wa mradi huo.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.