• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima afurahishwa na ziara ya walimu kutoka Zanzibar.

Posted on: February 10th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amefurahishwa na ziara ya Maafisa elimu na walimu Wakuu kutoka visiwani Zanzibar ziara iliyolenga kupata uzoefu katika nyanja mbalimbali za elimu ikiwemo usimamizi wa miradi ya elimu, taaluma pamoja na kudumisha muungano wa Zanzibar na Tanganyika.

Mhe. Malima ameyasema hayo Februari 10 mwaka huu wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya Maafisa Elimu hao kilichofanyi kakatika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kwake ni faraja kuona miaka 60 ya Mapinduzi walimu kutoka Zanzibar wanafika kufanya ziara ya mafunzo Mkoani humo na kubainisha kuwa Walimu hao wameongeza kitu kwa walimu wa Mkoa huo.

"...na leo miaka 60 ya Mapinduzi kuona walimu mmekuja kama hivi kwa kujitolea na kufanya ziara ya mafunzo kwangu mimi ni fahari kubwa sana yaani nimejisikia faraja sana...nimejifunza jambo kubwa sana..." amesema sisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha, amesema kuwa nchi hizo mbili zina malengo mbalimbali yanayofanana kwenye sekta ya elimu  ikiwemo kuongeza ufaulu wa wanafunzi na kufuta daraja sifuri, kudhibiti utoro na changamoto ya uhaba wa walimu wa masomo ya Sayansi na kusema kuwa Mkoa unaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa malengo hayo yanafikiwa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Adam Kighoma Malima amewasisitiza walimu hao kuzingatia masuala ya lishe kwa watoto ili kuondoa hali ya udumavu pia amewataka kusimamia maadili ya watoto na kupiga vita utamaduni wa kigeni ambao unasababisha mmomonyoko wa maadili hapa nchini.

Naye Afisa Elimu Sekondari kutoa Mkoa wa Kusini - Pemba Bw. Seif Mohammed Seif amesema lengo la ziara hiyo ni kujifunza mambo mbalimbali kwenye sekta ya elimu Mkoani humo ikiwemo uboreshaji wa taaluma na usimamizi wa miradi ya elimu huku akiusifu Mkoa wa Morogoro kwa kutekeleza miradi ya elimu kwa fedha za mapato ya ndani na kwamba wamefurahiswa na jambo hilo na wanakwenda kulifanyia kazi.

Aidha, amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Morogoro kwa kuweka mikakati mahususi ya kudhibiti nidhamu na utoro shuleni kupitia uhamasishaji wa utoaji wa chakula mashuleni na lishe kwa wanafunzi wake.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.