• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AZIPONGEZA SIMBA, YANGA KUTINGA ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA AFRIKA.

Posted on: March 6th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amezipongeza timu za Simba na Yanga kwa kuingia hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika huku akibainisha kuwa jambo hilo limeipa heshima nchi na kuitangazaTanzania kwa kuingiza timu mbili katika hatua hiyo.

Mhe. Malima ametoa pongezi hizo Machi 6, 2024 wakati akizungumza na baadhi ya viongozi wa timu ya Simba SC akiwemo Mtendaji Mkuu wa timu hiyo Bw. Imani Kajula ambao walifika ofisini kwa Mkuu huyo wa Mkoa kumtembelea.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema, Tanzania kupeleka timu mbili kwenye hatua ya robo fainali kwenye mashindano hayo ni kutokana na uwekezaji uliofanywa kwenye sekta ya michezo hapa nchini pamoja na uongozi imara wa nchi na timu hizo.

“...mimi kama mdau wa mpira wa miguu naomba niwapongeze sana na niwashukuru mmetuheshimisha...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Malima akisisitiza suala la michezo kwa jumla amesema, kuna haja ya kukuza vipaji vya ndani ya nchi ili kwa siku za baadaye nchi iwe na wachezaji wengi wa ndani na wengine wapate nafasi ya kucheza timu za nje.  

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa Mkoa utafanya kila jitihada katika kuendelea kuboresha uwanja wa Jamhuri ili uweze kufanana na uwanja wa Benjamini Mkapa na kuwaomba viongozi wa timu hizo kumshika mkono ili jambo hilo lifanikiwe.

Naye, Mtendaji Mkuu wa timu ya Simba SC Bw. Imani Kajula kwa niaba ya Uongozi na wachezaji wa timu hiyo, amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa maandalizi na mapokezi ya timu hiyo na kuongeza kuwa timu ya Simba itatumia uwanja wa Jamhuri kama uwanja wa nyumbani kwa michezo mitano wakianza na mchezo wao dhidi ya timu ya Tanzania Prisons utakao chezwa katika uwanja wa Jamhuri Machi 6, 2024.

Bw. Imani Kajula amemuhakikishia Mkuu huyo wa Mkoa kuwa watamsaidia kufanikisha dhamira yake ya kuboresha uwanja huku akiweka bayana kuwa timu yao ina wachezaji wengi wa timu B vijana kutoka mkoani Morogoro ambao baadae watakuwa tishio na kuahidi kurudi  tena mkoani humu rasmi kwa ajili ya kuunga mkono juhudi zinazofanyika katika kukuza vipaji.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.